TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, November 21, 2014

Rais kutoa msamaha kwa wafungwa Waandishi wa Habari

pingu
Waandishi wa habari watatu walioshtakiwa kwa kuandika habari za kichochezi huenda wakaachiwa huru hivi karibuni kwa msamaha wa Rais.
Waandishi wa Habari hao Peter Greste raia wa Australia, Mohammed Fahmy mwenye asili ya Canada na Baher Mohammed wanashikiliwa Misri ambako walihukumiwa kifungo baada ya kukutwa na hatia ya kukisaidia chama cha Muslim Brotherhood na kueneza habari za kupendelea upande wa Kikundi hicho.
Mohammed Fahmy, Peter Greste, Baher Mohamed
Rais wa Misri, Abdi Fatah El Sisi amesema msamaha huo utatolewa kama hakutakuwa na athari yoyote kwa nchi hiyo kiusalama.
Waandishi wawili kati yao walihukumiwa kifungo cha miaka 10, mmoja wao akihukumiwa kifungo cha miaka 7.

No comments:

Post a Comment