TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, November 20, 2014

Mapya kuhusu huduma za chakula Mgahawa wa Bunge

Mjengo 
…Naomba mwongozo wako kwamba kinachoendelea katika viwanja hivi vya Bunge pale Kantini,  kuna mabadiliko makubwa sana yamefanyika kwa watoa huduma kiasi kwamba kwanza hata huduma zao na kauli zao kwa wateja wao sisi wabunge sio nzuri..“, Hiyo ilikuwa kauli ya mwongozo wa Mbunge Martha Mlacha alipopewa nafasi kutoa mwongozo wake katika kikao cha Bunge leo Dodoma.
…Lakini kitu ambacho.. ninachokuomba mwongozo  kwamba Bunge hili.. hapa mahali hapa.. ndiyo chimbuko na kisima cha watetea haki za Watanzania wote, wakiwemo vibarua, wafanyakazi na watu wengine na kwamba kama kuna kampuni inachukua ama kufanya biashara kwenye eneo fulani ikakuta wafanyakazi maeneo yale, inabidi wafanyakazi wa eneo lile wachukuliwe na kampuni ile inayokuja pale…”– Mlata.
…Kumetokea sintofahamu naomba mwongozo wako, hivi sasa vijana thelathini waliokuwa wanafanya kazi katika kwenye kantini ile wanarandaranda mitaani wanakutana na sisi wabunge wakituomba tuwasaidie hata hela ya kula, naomba mwongozo wako ni nini kimetokea?..”– Mlata.
Akijibu mwongozo huo Naibu Spika; “… Hili ambalo ameliongea Mheshimiwa Mlatha ni jambo la ndani.. ni jambo la kwetu sisi wenyewe, niwahakikishieni waheshimiwa Wabunge kwa kifupi sana kwamba jambo hili liko mikono salama ya tume ya huduma za Bunge, mabadiliko hayo ni kwa nia njema watumishi waliokuwa pale wengi wao wamekuwa deployed tayari maeneo mengine ya kazi..“– Ndugai.
…Nawapa majibu ya uhakika, zaidi ya robo tatu wameshakuwa deployed tayari na tulikuwa na kamati ya tume jana wala sio juzi na tumelizungumzia jambo hili , wako vijana wachache ambao bado hawajachukuliwa, na hao wachache watachukuliwa watapangwa katika maeneo mengine ya shughuli. Kwa hiyo liko mikono salama kabisa…“– Ndugai.

No comments:

Post a Comment