Papa ataka majadiliano na IS

Baba
 mtakatifu Francis ametaka milango ya majadiliano na kundi la wanamgambo
 wa dola ya kiislam iwe wazi ,ingawa hali ni mbaya na ya kutatiza katika
 maeneo wanako tekeleza mashambulio yao.
Papa 
Francis ameyasema hayo wakati akirejea mjini Rome, Italia,baada ya 
kulitembelea bunge la muungano wa jumuiya ya Ulaya lilifanyika katika 
mji wa Strasbourg, Papa pia amesisitiza makubaliano ya kimataifa 
kutokomeza ugaidi yalikuwa muhimu.na hakuna ulazima wa nchi kupigana na 
ugaidi ikiwa peke yake nguvu ya pamoja ni muhimu sana.
Akilihutubia
 bunge hilo ,alishusha mvua za lawama kwa muungano huo kuwa una hatia 
kwa kuweka sheria zilizokuwa kali na za kuumiza, hasa katika suala la 
wahamiaji na kuonya kuwa Mediterranean isifanywe kuwa kaburi la 
wahamiaji wanaosafiri kwa boti kutokea upande wa kaskazini mwa Africa.CHANZO:BBC
No comments:
Post a Comment