TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, November 26, 2014

Papa ataka majadiliano na IS 


Baba mtakatifu Francis ametaka milango ya majadiliano na kundi la wanamgambo wa dola ya kiislam iwe wazi ,ingawa hali ni mbaya na ya kutatiza katika maeneo wanako tekeleza mashambulio yao.
Papa Francis ameyasema hayo wakati akirejea mjini Rome, Italia,baada ya kulitembelea bunge la muungano wa jumuiya ya Ulaya lilifanyika katika mji wa Strasbourg, Papa pia amesisitiza makubaliano ya kimataifa kutokomeza ugaidi yalikuwa muhimu.na hakuna ulazima wa nchi kupigana na ugaidi ikiwa peke yake nguvu ya pamoja ni muhimu sana.
Akilihutubia bunge hilo ,alishusha mvua za lawama kwa muungano huo kuwa una hatia kwa kuweka sheria zilizokuwa kali na za kuumiza, hasa katika suala la wahamiaji na kuonya kuwa Mediterranean isifanywe kuwa kaburi la wahamiaji wanaosafiri kwa boti kutokea upande wa kaskazini mwa Africa.CHANZO:BBC

No comments:

Post a Comment