TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, November 20, 2014

Baada ya Shy-Rose Bhanji kudaiwa kumpiga mbunge mwenzake, hiki kimesemwa bungeni

1 (1) 
Kumekuwa na taarifa kuhusu kuwepo migogoro mbalimbali inayohusisha Wabunge wawakilishi wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki ambapo Mbunge Shy-Rose Bhanji amehusishwa sana kwenye vichwa vya habari.
Kwenye kikao cha Bunge November 20 2014 Dodoma Hatibu ambae ni mbunge wa Zanzibar aliuliza >>> “… Sisi wabunge wa bunge hili ndiyo wapiga kura wa kuwachagua wawakilishi wetu wa kutuwakilisha katika bunge la Afrika Mashariki, kumekuwa na taarifa za kulipaka Taifa hili matope kulitia aibu kutokana na  baadhi ya wawakilishi wetu, Wabunge wetu wa Afrika Mashariki kutokana na matendo wanayoyafanya kule..
…Ni lini hasa kinachoendelea pale na hatua gani zilizochukuliwa kuhusu ukosefu wa nidhamu uliojitokeza kwa mbunge Shyrose Banji wazi wazi na bili hali hakuna taarifa yoyote, Mheshimiwa Naibu Spika naomba mwongozo wako…”– Hatibu.
Baada ya swali waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akawasha kipaza sauti na kutoa haya majibu “…Naomba nitoe taarifa kwamba kinachotokea katika Bunge la Afrika Mashariki kwa kiasi kikubwa kinahusu mgogoro wa  spika mwenyewe, hilo ndiyo chanzo cha matatizo mengi, kwa hiyo  wabunge  wa Bunge la  Afrika Mashariki wamegawika kataka makundi mawili, kuna kundi linalotaka Spika lazma aondolewe, na wengine wanadai wanamtetea abaki…
EA..
Sasa katika kundi ambalo wanataka  abaki imeonekana Tanzania ndio kikwazo, kwa sababu ili upate uamuzi ndani la Bunge la Afrika Mashariki  katika suala lolote lazima upate akidi inayotosheleza kutoka  kila nchi, sasa wabunge wa Tanzania ambao mwanzoni waliunga mkono hoja ya kumuondoa yule Spika wamefuta hilo na wamekubaliana aendelee kwa hiyo imeleta chuku kiasi Fulani…“– Sitta.
 “…Katika tukio ambalo limetokea juzi na nasema hivi kwa sababu  Naibu Waziri wangu yuko kule kwa hiyo ni jambo halisi, kilichotokea sio kama kinavyoelezwa Mheshimiwa Shyrose Banji ambaye anahesabika ni mfuasi mkubwa wa Yule Spika kiasi kwamba wenzie wanamuona kama kibaraka vile, alikuwa anapita katikati ya Wabunge wengine kuwahi usafiri kwa bahati mbaya akamgonga Mheshimiwa Ndelakindo Kessy, Mheshimiwa Ndelakindo akahamaki na kwa kusaidiwa na  baadhi ya Wabunge  wengine wa Uganda akaenda kituo cha Polisi kutoa taarifa kwa madai kwamba amefanyiwa makosa ya jinai wanaita ‘assaults’…“– Sitta.
“>…Ikabidi aitwe ‘Sergeant at Arms’ wa Bunge la EALA ambaye alikwishaanza jitihada za kulifanya jambo lile liishie ndani ya Bunge na katika jitihada hizo alifika mbali kidogo akawezesha Wabunge wetu hao wawili waweze kusikilizana na ninavyotoa taarifa hivi sasa ni kwamba jana suala hili limekwisha na haliendelezwi na Polisi tena…
“– Sitta.
Hivi ndivyo Waziri Sitta alimalizia kujibu suala hilo; “…Sasa yale mengine yaliyosema kwamba alifanya mambo ya hovyo Mheshimiwa yule tena kama miezi miwili iliyopita, bado yako mikononi mwa tume ya Bunge la Afrika Mashariki hadi hapo watakapolishughulikia hatuwezi kufanya kitu chochote, na tukishapata taarifa ya tume ya Bunge la Afrika Mashariki basi mimi nitatoa taarifa kwa Mheshimiwa Spika ili sasa sisi kwa wote kama jimbo la uchaguzi La Wabunge hao tuone ukweli ni upi na tujue hatua ya kuchukua..”– Sitta.

No comments:

Post a Comment