TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, November 27, 2014

U Heard ya Novemba 27 iko hapa, Steve Nyerere amjibu Linex kuhusiana na gari analodai kudhulumiwa

IMG_4502 
U Heard ya jana alisikika Linex ambaye alilalamika kudhulumiwa pesa kiasi cha milioni 11 na Nyamihela, ambaye alikutanishwa na muigizaji Steve Nyerere ambapo Linex alisema lengo lake ilikuwa ni kununua gari na Steve alimkutanisha na huyo jamaa kwa ajili ya kufanya biashara hiyo.
Leo amesikika Steve Nyerere ambapo amesema yeye aliwakutanisha Linex na Nyamihela baada ya Linex kumwambia kwamba anahitaji kununua gari, lakini baada ya hapo hakuwa na mawasiliano tena na Linex.
Steve amesema Linex alimtafuta baada ya kushindwana na Nyamihela na kumlalamikia Steve kwamba Nyamihela kamdhulumu pesa ambayo alimpatia ili amuuzie gari, japo Steve amesema kiasi cha pesa alichopatiwa Nyamihela ni milioni tatu na alimrudishia milioni moja kati ya pesa hizo.

No comments:

Post a Comment