Jeshi la Kenya kuwasaka wauaji Mandera mpakani mwa Somalia
Bus lililotekwa na wapiganaji wa Al shabab kabla ya kuwaua abiria 28 wasiokuwa waislamu,Mandera mpakani mwa Somalia
Na Martha Saranga Amini
Mshauri 
wa juu wa raisi Uhuru Kenyata Abdikadir Mohammed ametoa wito kwa wakenya
 wote wa imani zote kuungana pamoja dhidi ya wahalifu.
Hatua 
hiyo inakuja kufuatia mauaji ya alfajiri ya jana kutekelezwa na 
wapiganaji wa kiislamu kutoka somalia ambao waliteka basi moja na kuwaua
 abiria ambao hawakuwa waislamu.(P.T)
Tayari 
maafisa wa jeshi la Kenya KDF wamewasili Mandera eneo la mpakani mwa 
somalia kuwasaka waliotekeleza mauaji hayo na kuhakikisha ulinzi baada 
ya abiria 28 kuuawa mapema jana.
Kundi la 
Al-Shabab limesema shambulizi hilo lililenga kulipa kisasi kufuatia 
mauaji ya waislamu ambayo kundi hilo limedai kutekelezwa na majeshi ya 
kenya katika mji wa pwani wa Mombasa.
Serikali ya kenya imesema imeanza kuwatambua wahalifu hao na itahakikisha inafikisha mbele ya sheria.
Waziri wa
 mambo ya ndani Joseph Olellenku amesema kuwa kambi iliyokuwa 
inamilikiwa na wapiganaji hao huko mandera imeshambuliwa na jeshi la 
kenya.
Chanzo:RFI
No comments:
Post a Comment