TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, November 20, 2014

Taarifa nyingine kuhusu Cosby baada ya kukabiliwa na tuhuma za kubaka

 images ii Kwa zaidi ya wiki moja sasa kama umekuwa mfuatiliaji wa vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa kumekuwa na taarifa kuhusu tuhuma za kubaka zinazomkabili mchekeshaji wa Marekani, Mzee Bill Cosby.

Kituo cha NBS ambacho kilikuwa kikifanya kazi na mzee huyo, kimesitisha kuirusha show yake kutokana na tuhuma hizo zinazomkabili kwa mujibu wa msemaji wa kituo hicho, Rebecca Marks.
Tuhuma hizo zilitolewa na mwanamitindo ambaye pia ni mtangazaji wa Televisheni, Janice Dickinson ambaye amesema mwaka 1982 Cosby alimnywesha pombe kabla ya kumfanyia kitendo hicho.
Mwanamke huyo amesema alishindwa kuripoti Polisi baada ya kufanyiwa kitendo hicho kwa kuwa alihisi hakuna ambaye angeweza kumuamini.
Mwanasheria wa Cosby amepinga madai hayo japo Cosby  mwenyewe hajazungumzia lolote mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment