Kiemba aanza kupiga kazi Azam

Amri Kiemba
AMRI 
Kiemba ataanza mazoezi kwenye kikosi chake kipya cha Azam FC leo 
Jumatatu, lakini ametoa la moyoni kwa kusema, yaliyomtokea Simba 
hayamuumizi kichwa na anayachukulia kama sehemu ya changamoto na sasa 
ametua kwa Bakhresa kila kitu amemwachia Mungu ili aamue hatma yake.
Lakini 
akaenda mbali na kuwaambia mabosi wake wa sasa, yeye hajui kuchagua, 
wampe jezi yenye namba yoyote ile iliyopo au watakayoona inamfaa 
ataivaa.
Kiemba amekwenda Azam kwa mkopo na dau la Sh10 milioni akitokea Simba.(P.T)
Mchezaji 
huyo ameliambia Mwanaspoti kuwa: "Tukijaaliwa kesho (leo) nitaanza 
mazoezi rasmi. Binafsi nimejiandaa vizuri lakini siwezi kutoa ahadi 
nyingi kila kitu nimemwachia Mungu aamue."
"Unajua 
wakati mwingine binadamu tunakosea, unasema nitafanya hiki na hiki 
lakini utambue kuwa yote yanapangwa na Mungu kikubwa naomba 
ushirikiano,"alisema Kiemba ambaye amebakiza miezi sita Simba na 
amekwenda kwa mkopo Azam kwa miezi sita.
"Unaweza kukuta, hata hicho kilichonitokea Simba, ilipangwa tu ili kifanyike hiki kilichofanyika."
Akizungumzia sakata lake Simba, Kiemba alisema:
"Yote 
nayachukulia kawaida tu kuwa ni sehemu ya changamoto za maisha, ndivyo 
ilivyokuwa imepangwa, sitaki kuyazungumzia sana kwa undani."
Hadi 
kutua kikosini hapo, Kiemba alikuwa amesimamishwa na uongozi wa Simba 
kwa kile kinachodaiwa ni utovu wa nidhamu. Alisimamishwa pamoja na 
wachezaji wenzake, Shaaban Kisiga 'Marlone' na Haroun Chanongo.
Chanzo:Mwanaspoti
No comments:
Post a Comment