WAHABESHI 22 WAKAMATWA DAR

RAIA 22 wa Ethiopia wanashikiliwa na Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam kwa tuhuma za kuingia nchini bila kibali.
Akizungumza
 na Tanzania Daima ofisini kwake jana, Ofisa Uhamiaji Mkoa, Grace 
Hokororo, alisema Wahabeshi hao walikamatwa juzi usiku katika maeneo ya 
Kinondoni wakiwa katika pagale ambamo walikuwa wamejificha.(HD)
Alisema baada ya wananchi kuwaona waliwatilia mashaka na ndipo walipotoa taarifa polisi ambao walifika na kuwakamata.
"Hii hali
 ilikuwa imepoa lakini hivi sasa naona tena wameibuka kwa kweli kazi ipo
 na hawa tunategemea kuwasafirisha na kuwarudisha kwao wakiwemo 
Wanyarwanda tisa,'' alisema Hokororo.
Alisema 
wiki tatu zilizopota jumla ya wahamiaji 42 wakiwemo Wahabeshi, Wasomali 
na Wanyarwanda walisafirishwa na kurudishwa makwao.
Alisema 
pamoja na jitihada za idara hiyo kuwakamata raia hao, inakabiliwa na 
changamoto ya upungufu wa watumishi na magari, jambo alilosema limekuwa 
likikwamisha jitihada za idara hiyo katika kutekeleza majukumu yake.
"Watumishi
 wengi wamechukuliwa na NIDA na hapa nimebakiwa na wachache na magari 
pia ni tatizo tunaiomba serikali iliangalie na ione umuhimu wa 
kutuongezea watumishi ili tuweze kufanya kazi vizuri," alisema.
No comments:
Post a Comment