TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, November 11, 2013

Taarifa kuhusu Watuhumiwa waliomvamia Dr. Sengondo Mvungi

Sengondo Mvungi 1
Watuhumiwa tisa wanaotajwa kuhusika katika tukio la kuvamia, kuiba na kumjeruhi mjumbe wa tume ya kukusanya na kuratibu maoni ya katiba mpya Dr. Sengondo Mvungi, wanashikiliwa na jesi la polisi Dar es salaam wakiwa na kidhibiti cha mapanga matano yaliyotumika kutekekeleza uhalifu huo.
Waziri wa mambo ya ndani Dr. Emmanuel Nchimbi amesema pamoja na mapanga, watuhumiwa hao wamekutwa na simu moja iliyoibiwa siku ya tukio pamoja na kigoda ambacho kilitumika kufanikisha hilo zoezi.
Alietajwa kuhusika zaidi kwa kupanga tukio lenyewe ni fundi ujenzi Msigwa Mopela aliejenga nyumba ya Dr. Mvugi ambapo Chibago Magosi nae alishirikiana na fundi huyu.
Waziri Nchimbi anasema kuhusu kutokamilika kwa upelelezi wa matukio mengine ya kujeruhi na kutekwa likiwemo la Dr. Steven Ulimboka pamoja na tukio la kuvamiwa kwa Mhariri mtendaji wa gazeti la Mtanzania Absaloom Kibanda, Dr. Nchimbi amesema matukio yanatofautiana.
Kukamatwa kwa Watuhumiwa hawa kumetokea siku nane baada ya kujeruhiwa kwa Dr. Mvungi aliyeko nchini South Africa kwa ajili ya matibabu.

No comments:

Post a Comment