NIDA:WATENDAJI WANAODAI FEDHA ZA VITAMBULISHO KUKIONA

Mamlaka 
ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), imewaonya baadhi ya watendaji wa mitaa
 jijini Dar es Salaam wanaodaiwa kuwatoza fedha wananchi kwa ajili ya 
kuwapatia vitambulisho hivyo na kwamba wakibainika watachukuliwa hatua 
za sheria.(HD)
Aidha, 
imesema zoezi la utaoji wa vitambulisho limefikia katika hatua ya 
kuchukua alama za vidole na picha kwa watu waliojaza fomu za kuviomba.
Mkurugenzi
 Mkuu wa Nida, Dickson Maimu, akizungumza katika mahojiano na Radio One,
 alisema zoezi la vitambulisho linagharamiwa na serikali kwa asilimia 
100, hivyo hairuhusiwi mtendaji yeyote kumtoza fedha mwananchi.
Alisema 
zoezi linaendelea katika wilaya za Jiji la Dar es Salaam na Zanzibar na 
kuwa wanaopuuza kupata vitambulisho vya taifa watapata athari ikiwamo 
kushindwa kupata huduma mbalimbali kama kufungua akaunti au kupata 
ajira.
Kuna 
madai kuwa baadhi ya watendaji wa mitaa katika jijini Dar es Salaam 
wamekuwa wakiwatoza Sh. 2,000 watu wanaokwenda katika ofisi zao ili 
kugongewa mihuli.
CHANZO: NIPASHE
No comments:
Post a Comment