TUCTA YATAKA SH.750,000 KIMA CHINI

Shirikisho
 la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta) Mkoani Mbeya, limetangaza kiwango 
kipya cha mishahara inayotakiwa kuwa kima cha chini ni Sh 750,000.(HD)
Mwenyekiti
 wa Tucta mkoani hapa, Alinanuswe Mwakapala alisema kwa maisha ya sasa 
kima cha chini lazima kiwe Sh750,000 na kwamba, pendekezo hilo la mkoa 
litawasilishwa kwenye ngazi za juu za Tucta ili kulibariki.
Mwakapala
 alisema hayo kwenye hafla ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT) 
kukabidhiwa jengo la ghorofa tano lililojengwa na Jeshi la Kujenga Taifa
 (JKT).
"Wafanyakazi
 nchini sasa wamechoshwa na mishahara midogo, hivyo wakati umefika kwa 
wafanyakazi kutoogopa maandamano na migomo kudai haki," alisema huku 
akishangiliwa.
Hata 
hivyo, Rais wa CWT, Gratius Mukoba alisema madai ya wafanyakazi 
yaliyowasilishwa Serikalini ni kutaka nyongeza ya mishahara kwa asilimia
 100.
Mkoba alisema CWT hivi sasa wanasubiru ndani ya miezi mwili hadi Desemba kupata majibu.
hayatapatikana basi Serikali ijue imejipalia mkaa.
''Hatuwezi
 kuendelea kuwaona watu wasiofanyakazi wanapata mishahara mikubwa wakati
 wafanyakazi wanasota. Mwisho wa matatizo hayo ni sasa'' alisema huku 
akiwataka wafanyakazi hususan walimu kuachana na njama za kutaka 
kuwatenganisha.
Alisema 
Serikali inatakiwa kuwalipa walimu Sh49 bilioni wanazodai zikiwamo Sh30 
bilioni walizopunjwa katika mishahara na kwamba pia lazima ipunguze kodi
 kwa wafanyakazi na kuboresha mazingira ya kazi.CHANZO MWANANCHI
No comments:
Post a Comment