HAWA NDIO MABILIONEA WANNE VINARA TANZANIA

Mfanyabiashara maarufu nchini, Rostam Aziz (49), ametajwa kuwa ndiye tajiri namba moja Tanzania kwa sasa.
Kwa 
mujibu wa utafiti uliofanywa na Jarida la Marekani la Forbes na kutoa 
taarifa yake juzi, Rostam amekamata nafasi hiyo na ya 27 katika Afrika 
akiwa na utajiri wa Dola za Marekani bilioni moja Sh1.6 trilioni.(HD)
Mbunge 
huyo wa zamani wa Igunga, ameingia kwa mara ya kwanza katika orodha ya 
matajiri 50 wa Afrika ya jarida hilo, pamoja na wafanyabiashara wengine 
wa Tanzania, Reginald Mengi na Mbunge wa Singida Mjini (CCM), Mohamed 
Dewji 'Mo'. Katika orodha hiyo pia yumo Said Bakhresa ambaye aliwahi 
kutajwa siku za nyuma.
Rostam, 
ambaye aliachana na siasa mwaka 2011, amempiku Bakhresa, ambaye mwaka 
jana Jarida la Ventures Africa la Nigeria lilimtaja kuwa ndiye aliyekuwa
 tajiri namba moja wa Tanzania. Bakhressa katika kipindi hicho 
alikadiriwa kuwa na utajiri wa Dola 620 milioni (Sh971 bilioni).
Katika orodha hiyo ya Ventures Africa, Bakhresa alifuatiwa na Rostam, Mengi na mfanyabiashara mwingine maarufu, Ali Mufuruki.
Mengi anashika nafasi ya pili kwa Tanzania na ya 34 Afrika akiwa na utajiri wa Dola 550 milioni (Sh861 bilioni).
Forbes 
linaonyesha kuwa Bakhresa amefungana na Mo katika nafasi ya tatu ya 
orodha ya matajiri wa Tanzania na ya 38 kwa Afrika, wote wakiwa na 
utajiri wa Dola 500 milioni (Sh783 bilioni).
Rostam, 
Mengi na Bakhresa hawakupatikana jana kuzungumzia suala hilo huku Mo 
akisema kwamba asingeweza kuzungumzia suala hilo kwa kuwa jana alikuwa 
katika mapumziko ya Sikukuu ya Ashura.
Tajiri wa
 Nigeria, Aliko Dangote, ambaye anajenga Kiwanda cha Saruji huko Mtwara 
ndiye anayeshika nafasi ya kwanza katika orodha ya Afrika, akiwa na 
utajiri wa Dola20 bilioni (Sh31.7 trilioni), akifuatiwa na familia ya 
Johanny Rupert ya Afrika Kusini yenye utajiri wa Dola7 bilioni (Sh10.7 
trilioni) na Nick Oppenheimer, pia wa Afrika Kusini mwenye utajiri wa 
Dola 6.6 bilioni (Sh10.3 trilioni).
1)Rostam Aziz
Jarida la
 Forbes limeripoti kuwa utajiri wa Rostam unachangiwa zaidi na biashara 
ya mawasiliano ya simu za mkononi, ujenzi na uchimbaji wa madini.Pia 
anamiliki Kampuni ya Caspian, ambayo inafanya kazi za kuchimba madini 
katika migodi inayomilikiwa na Kampuni za BHP Billiton na Barrick Gold.
Pia ana 
hisa katika Kampuni ya Hutchison Wampoa inayofanya kazi za kupakua 
mizigo bandarini na anamiliki majumba nchini na katika nchi za Mashariki
 ya Kati.
2) Mengi
Ni Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za IPP.
Utajiri wake unatokana na kumiliki vyombo vya habari, kiwanda cha vinywaji baridi na madini.
Mengi anamiliki magazeti kumi na moja, vituo vitatu vya televisheni na takriban vituo 10 vya redio.
Pia ana mgodi wa madini ya dhahabu na viwanda vya CocaCola.
Kwa mujibu jarida hilo, Mengi alizaliwa katika familia maskini na baadaye kusomea uhasibu huko Uingereza na kufanya kazi huko.
Alijiunga
 na Chama cha Wahasibu cha Uingereza kabla ya kurejea Tanzania mwaka 
1971 na kuajiriwa na Kampuni ya Ukaguzi ya Coopers & Lybrand 
Tanzania (sasa Price Water House Coopers) hadi mwaka 1989, alipoacha 
kazi na kujikita zaidi katika biashara.
3) Bakhresa
Said 
Salim Bakhresa ni mwasisi na Mwenyekiti wa Kampuni ya Bakhresa Group na 
ana utajiri wa Dola500 milioni (Sh783 bilioni).Bakhresa aliacha shule 
akiwa na umri wa miaka 14 na kuanza biashara ya kuuza viazi mbatata. 
Baada ya hapo alifungua mgahawa na baadaye kuingia katika biashara ya 
kusaga nafaka.
4) Mo
Mafanikio
 yake yamechangiwa zaidi baada ya kuendeleza mali ya wazazi wake. 
Anafanya biashara ya nyumba, kuuza mazao na viwanda vya mafuta.
Mo 
alirejea Tanzania baada ya kumaliza masomo yake katika Chuo Kikuu cha 
Georgetown, Marekani na kuendeleza biashara ya maduka ambayo 
yalianzishwa na baba yake.
Alinufaika baada ya kununua viwanda vilivyobinafsishwa na Serikali.
Alivifanya
 viwanda hivyo kutengeneza faida na kuinyanyua Kampuni ya Mohamed 
Enterprises (MeTL) kuwa miongoni mwa kampuni zenye mafanikio makubwa 
Tanzania.
Mo pia anajihusisha na biashara ya usambazaji bidhaa, viwanda vya nguo na kilimo.
Jarida 
hilo lilipiga hesabu za utajiri wa wafanyabiashara hao kwa kuangalia 
thamani ya bidhaa zinazouzwa na kampuni zao, mikataba yao na hasa wale 
walio kwenye sekta ya mafuta na ukubwa wa kampuni zao.CHANZO MWANANCHI
No comments:
Post a Comment