LOWASSA:TULIOHUZUNIKA,TUTASHINDA PAMOJA

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema waliofurahi na kuhuzunika naye pia watashinda pamoja naye.
Bila 
kufafanua kauli yake jana, Lowassa aliwaambia wakazi wa Monduli mkoani 
Arusha kuwa: "Kumbukeni kaulimbiu yangu wakati wa Uchaguzi Mkuu 
uliopita, tulifurahi pamoja, tulihuzunika pamoja na tutashinda pamoja".(HD)
Mbunge 
huyo wa Monduli alikuwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mara baada
 ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa wodi mbili za ghorofa za wazazi 
katika Hospitali ya Wilaya ya Monduli.
Katika 
hotuba yake fupi, pia alitamba kwamba atayashinda majaribu. Hata hivyo, 
hakufafanua majaribu hayo... "Kuna vita kubwa, lakini ambacho naweza 
kusema ni kuwa nayaweza yote kwa yeye anitiaye nguvu."
Kuhusu 
afya yake ambayo mara kadhaa imeelezwa kuwa siyo imara, kiongozi huyo 
alisema kwa sasa ni nzuri na imeimarika kupita kipindi kingine chochote.
Lowassa 
alisema kuanza ujenzi wa majengo hayo ambayo ni utekelezaji wa ahadi 
zake, ni moja ya ushindi na kuwataka wakazi wa Monduli, kumshukuru Mungu
 kwa yanayotokea.
Mwenyekiti
 wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Onesmo Nangole aliwataka wakazi wa Monduli, 
kumshukuru Mungu kwa kuwa na mbunge Lowassa ambaye anapendwa nchi nzima.
"Monduli 
Mungu awape nini, Lowassa anaitwa kila mahala kusaidia kutokana na moyo 
wake wa huruma na hapa ametekeleza ilani yote ya uchaguzi," alisema.
Kauli ya 
Lowassa imekuja siku chache tangu mtangulizi wake katika nafasi ya 
Waziri Mkuu, Frederick Sumaye alipomtuhumu hadharani kwamba amekuwa 
akimhujumu na kumwekea vikwazo vya kisiasa kwa kutumia mbinu chafu. 
Miongoni mwa mambo yaliyoonekana kumkera Sumaye ni habari iliyoandikwa 
na gazeti hili Septemba 16, mwaka huu inayohusu mradi wa maji Ziwa 
Victoria, ambayo Lowassa alinukuliwa akisema kuwa wakati akiwa Waziri wa
 Maji, aliungwa mkono na mawaziri watatu tu alipopendekeza mradi huo wa 
maji.
Sumaye 
alisema: "Najua mhusika ametumia sana mradi huu kisiasa na sisi wengine 
tumenyamaza japo ukweli tunaujua. Amenilazimisha niseme ukweli kuhusu 
mradi huu kwa sababu mimi nilikuwa Waziri Mkuu na mradi umetekelezwa 
chini ya uangalizi wangu," alisema na kuongeza:
"Kama 
waziri anaweza kubuni na kutekeleza mradi mkubwa hivyo peke yake, sasa 
akiwa Waziri Mkuu si maji yangefika Dodoma? Mbona hata bado kuna sehemu 
za Kanda ya Ziwa bado kuna shida ya maji?"
Tangu 
Sumaye atoe tuhuma hizo ambazo zinahusishwa na vita ya kuwania urais wa 
2015, Lowassa hakuwahi kujibu chochote wala kusikika akizungumza 
hadharani, hadi jana.Lowassa alisema mafanikio yaliyopatikana katika 
jimbo lake na mengine nchini, yanatokana na utekelezaji wa Ilani ya 
Uchaguzi ya CCM, ambao umefanywa na Rais Jakaya Kikwete.
"Hakuna 
kipindi ambacho ilani ya uchaguzi imetekelezwa kwa kiasi kikubwa kama 
kipindi cha Rais Kikwete naomba sote tumpongeze," alisema Lowassa.
Alisema 
hivi karibuni amekutana na Rais Kikwete ambaye ametoa Sh3 bilioni za 
ujenzi wa mabwawa 10 katika wilaya hiyo ili kukabiliana na tatizo la 
maji.
Wodi hizo
 za kisasa zinajengwa na Kampuni za Meelo Constraction na Bulem 
Constraction za Arusha kwa gharama ya Sh1.9 bilioni na zitakuwa na uwezo
 wa kulaza wagonjwa 140 wakati mmoja.
No comments:
Post a Comment