TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, November 1, 2013

ICC YAAHIRISHA KESI DHIDI YA RAIS KENYETTA

 131013152443_addis_union_africaine_african_union_uhuru_kenyatta_12102013_304x171_reuters_nocredit_0143d.jpg

Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC imeahirisha kesi ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta katika mahakama hiyo hadi tarehe 5 mwezi Februari mwaka 2014.
Uamuzi huo umefikiwa hii leo ikiwa siku moja kabla ya upande wa mashitaka kuashiria kuwa hawatapinga ikiwa kesi hiyo kuahirishwa kwa mwaka mmoja hadi Novemba mwaka 2014
Pia unakuja huku juhudi za kidipmolasia za viongozi wa Afrika kushinikiza baraza la usalama la Umoja wa Mataifa zikishika kasi kulitaka baraza hilo kukubali kesi dhidi ya Rais Kenyatta na naibu wake William Ruto kuakhirishwa.(P.T)
Rais Kenyatta alikuwa ameiomba mahakama hiyo kuakhirisha kesi dhidi yake hadi Februari mwaka ujao huku upande wa mashitaka ukitaka ukahirishaji kutozidi Februari tarehe tatu mwaka 2014.
"Majaji wamekubaliana na upande wa mashitaka kuahirisha kesi dhidi ya Rais Kenyatta hadi Februari mwaka 2014 ili kuupatia upande wa mashitaka muda wa kutosha kufanya uchunguzi zaidi kutokana na tuhuma dhidi ya upande wa mashitaka kutoa taarifa zisizo za kweli, '' majaji walisema katika uamuzi wao.
Upande wa utetezi nao ulitaka tarehe ya kesi hiyo kuahirishwa ili majaji waweze kushughulikia baadhi ya malalamiko yao, kuhusu Kiongozi wa mashitaka kuhujumu mfumo wa kesi dhidi ya Kenyatta. Malalamiko hayo waliyawasilisha Oktoba tarehe kumi na kuwasilisha ombi la kutaka kesi dhidi ya Rais Kenyatta kufutiliwa mbali.

No comments:

Post a Comment