TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, November 5, 2013

MOYES AWATAKA MAREFA KUMLINDA JANUZAJ KAMA MESSI 

 janujaz 6b57f

KOCHA David Moyes amesema winga Adnan Januzai lazima alindwe na marefa baada ya Sascha Riether kuwa mchezaji wa kwanza kuadhibiwa chini ya sheria mpya baada ya marefa kutoona tukio uwanjani. (HM)

Mshambuliaji huyo kinda alikuwa alichezewa rafu na beki huyo wa Fulham, United ikishinda 3-1 Uwanja wa Craven Cottage Jumamosi.
Refa Lee Probert na wasaidizi wake hawakuona tukio hilo wakati linatokea, lakini marudio ya picha za video yanaonyesha vizuri.
Na kwa sababu huyo, beki huyo wa pembeni ameadhibiwa na FA kwa kufungiwa mechi tatu.
Inamaanisha Riether anakuwa mchezaji wa kwanza kuadhibiwa chini ya sheria mpya ya FA, kumuadhibu mchezaji ambaye alifanya kosa lakini halikuonekana kwa marefa wakat wa mechi. Chanzo: binzubeiry

No comments:

Post a Comment