MAKINDA AAMUA ‘UGOMVI’BAINA YA LUKUVI, ABWAO


Spika wa 
Bunge, Anne Makinda jana aliingilia kati mvutano baina ya Waziri wa 
Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi 
baada ya kubanwa na Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema) Chiku Abwao.
Hali hiyo
 ilijitokeza pale Lukuvi alipolazimika kutumia nafasi yake ya uwaziri 
kujibu swali la nyongeza lililoulizwa na Abwao kuhusu mpango wa serikali
 wa kufikisha maji Isimani. "Mheshimiwa Waziri, Jimbo la Isimani 
wananchi wake wana matatizo makubwa ya upatikanaji wa maji na wamekuwa 
na maisha magumu,hivyo wanahitaji msaada huo, je Serikali inatoa kauli 
gani kuhusu kuwasaidia wananchi hao," aliuliza Abwao.(P.T)
Akijibu 
swali hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen
 Wassira alisema shida waliyonayo wananchi wa Isimani ni sawa na maeneo 
mengine nchini .
Baada ya 
majibu hayo, Lukuvi alilazimika kusimama ghafla na kuwasha kipaza 
sauti,ili kusawazisha jibu la swali hilo ambalo lililenga moja kwa moja 
katika jimbo lake,Baadhi ya wabunge walianza kupiga kelele za kumtaka 
Lukuvi asizungumze kwa kuwa swali lilimlenga moja kwa moja.
No comments:
Post a Comment