Tanzania 
Daima limedokezwa kuwa mkakati huo unahusishwa na njama za kutaka 
kukibeba Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi huo kwa kuchakachua 
matokeo ya kukibakiza madarakani.
Kampuni 
hizo ambazo katika zabuni ya Tume ya Uchaguzi zimetajwa kushirikiana na 
Kampuni ya Kitanzania ya M/S SCI Tanzania Limited, mbali ya kutojulikana
 zinapotoka, pia ndizo zimekuwa na gharama kubwa kuliko kampuni nyingine
 zilizoomba kazi hiyo.
Kiwango 
ambacho kampuni hizo zilitaja na kukubaliwa na NEC kwa ajili ya kuandaa 
vifaa vya kielektroniki vya kusajili wapiga kura (Biometric Voters 
Registration) ni zaidi ya euro milioni 60, sawa na sh bilioni 126.3, 
wakati kampuni zinazofuata zikihitaji kuanzia euro milioni 40.
Naibu 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe,
 ni mmoja wa viongozi waliofichua mkakati huo, akidai unafanywa na 
serikali ya CCM ili kuhakikisha wanajiandaa kudhibiti kila eneo ili 
waweze kubaki madarakani.
Alisema 
lengo ni kuhakikisha mchakato wa vitambulisho vya kupigia kura vya 
kielektroniki vina kuwa na faida kwa CCM na kukiingizia fedha chama 
hicho za kutumia kwenye uchaguzi huo kupitia mfumo huo dhaifu wa 
vitambulisho hivyo.
Zitto 
alisema kutokana na hali hiyo, amemwandikia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa 
Serikali (CAG) barua ya kutaka ukaguzi wa zabuni hiyo ufanyike kwa 
kushirikisha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na 
vyombo vingine vya usalama kwa ajili ya kujiridhisha.
"Wenzetu 
CCM wanafanya mikakati ya kujiandaa na Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwa 
kuhakikisha wanapata fedha za kutosha na hata mazingira mabaya ya vifaa 
vitakavyotumika katika upigaji kura na sasa wameshaingia hata katika 
Tume ya Uchaguzi kwa ajili ya kutengeneza mazingira," alisema Zitto.
Aliongeza
 kuwa kiasi kilichotolewa ni kodi ya Watanzania na kwamba ni vema taifa 
likajiridhisha kuwa matatizo yaliyotokea Kenya na Ghana hayatajirudia 
Tanzania, hasa wakati wa upigaji kura.
Gazeti 
hili limeona barua hiyo ya Zitto kwenda kwa CAG, ya Novemba 7, 2013, 
yenye kichwa cha habari; 'Zabuni ya Biometric Voters Registration (BRV 
KITS) No. IE/018/2012-13/HQ/G/19 yenye thamani ya sh bilioni 126.3.'
Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini anasema kuwa NEC imekuwa katika mchakato wa zabuni tajwa hapo juu.
"Zabuni 
hiyo sasa imeanza kuleta malalamiko miongoni mwa wananchi kutokana na 
kinachosemekana kuwa kampuni iliyopewa zabuni hiyo haina uwezo 
kiteknolojia, pia bei zao ni kubwa.
"Katika 
mafunzo ya hivi karibuni ya SADCOPAC jijini Nairobi tuliazimia kuwa ni 
vema kwenye zabuni nyeti kama za namna hii, SAIs wawe na uwezo wa 
kufanya ukaguzi kabla ya zabuni kutolewa na kuanza kutekelezwa," 
alisema.
Kwa 
mujibu wa nyaraka za NEC ambazo Tanzania Daima linazo, kampuni 
zilizopewa tenda ya pamoja yenye kugharimu kiasi cha dola 78, 
987,636.00, sawa na sh 126,291,375,455 ni M/S Jazzmatrix Cooperation na 
M/S Invu IT Solution ambazo hazijulikani nchi zinapotoka zikiwa 
zinashirikiana na M/S SCI Tanzania Limited.
Katika 
nyaraka hizo kampuni zilizokosa tenda na ambazo zimelalamika kwa 
Mkurugenzi wa NEC namna mchakato wa kutoa zabuni hiyo ulivyoendeshwa 
zimeainishwa kuwa ni M/S Zetes SA ya nchini Ubalgiji, M/S IRIS 
Corporation Technology ya Malaysia, M/S Lithotech Exports ya Afrika 
Kusini, M/S Safran Morpho ya Ufaransa na M/S Avante International 
Technology, Inc ya Marerkani.
Kampuni 
hizo zinahoji njia na sababu zilizowafanya wakose tenda hiyo licha ya 
kuwa na uzoefu, vifaa bora pamoja na kuwa na kiwango kidogo cha gharama 
tofauti na kampuni iliyopewa kazi.
Katika 
moja ya malalamiko yao, Kampuni ya M/S Morpho, inalalamika 
kutofahamishwa namna walivyokosa vigezo vya kupata kazi hiyo licha ya 
kuwa na sifa za kimataifa za kufanya kazi huku ikiwa imetoa bei nafuu 
kuliko kampuni iliyopata kazi.
"Tulikuwa
 miongoni mwa washindani muhimu kwa kuwa kiwango chetu kilikuwa ni sh 
bilioni 97.8 ambazo ni sawa na euro 44,939,912 + sh 3,843,736,140.
"Ujuzi, 
vigezo na uzoefu wetu havilingani, duniani kote tumefanya kazi katika 
maeneo mengine kwa ufanisi na tunashindwa kuelewa kivipi walishinda hao 
ambao wamepata kazi kwa kiwango cha zaidi ya sh bilioni 27.8 
ikilinganishwa na yetu," ilisomeka sehemu ya barua.
Alipotafutwa
 Mkurugenzi wa NEC, Julius Mallaba, alisema hawezi kuliongelea suala 
hilo katika simu na kuomba mwandishi awasiliane na Kaimu Mkurugenzi wa 
NEC, Dk. Sist Cariah, ambaye alisema mchakato wa kupata kampuni 
ulifuatwa kisheria.
Dk. 
Cariah alisema si kweli kwamba kampuni iliyopewa kazi haina uwezo bali 
malalamiko yanatoka kwa watu walioshindwa kupata kazi hiyo.
Alipoulizwa
 juu ya uzoefu wa kampuni hiyo na wapi ilifanya kazi, Dk. Cariah alisema
 kwa maelezo waliyonayo ni kwamba kampuni hiyo ina uzoefu wa miaka 35 wa
 kufanya kazi, huku akishindwa kuainisha sehemu ilizowahi kufanya kazi.
Kuhusu 
wapi zimetoka kampuni hizo, Dk. Cariah alisema suala la kutoainishwa 
kimaandishi ni makosa ya kawaida, huku akitaja kuwa zinatoka katika nchi
 ya India na Australia.
Kuhusu 
gharama, Dk. Cariah alisema licha ya makampuni mengine kutaja gharama za
 chini, zingeweza kuwa na gharama kubwa zaidi wakati wa kukamilisha kazi
 hiyo kutokana na kuwa na gharama zilizojificha.(CHANZO TANZANIA DAIMA)