TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, July 12, 2013

BONDIA EVANDER HOLFIELD KUJA TANZANIA
.
Jay Msangi ambae anaonekana katikati ameshawahi kucheza ngumi akiwa anaishi Marekani.
Taarifa ikufikie kwamba yule bondia mkongwe ambae ni mmoja kati ya waliowahi kumiliki headlines za dunia sana Evander Holyfield anatarajiwa kuja Tanzania.
PromotaMtanzania Jay Msangi kutoka Hall of Fame Boxing and Promotions Company  ameongea na Millard Ayo na kumwambia hiyo game imepangwa kuchezwa Uwanja wa Taifa April 27 2014 Uwanja wa Taifa ambapo Evander atapigana na Francois Botha wa South Africa aliewahi kuwa bingwa mara mbili.
.
Evander na Francois
Jay amesema haijawa ngumu kumpata Evander kwa ajili ya pambano kwa sababu kampuni yake ina uzoefu wa miaka mingi na imeshaandaa mapambano zaidi 30 kwenye jimbo la Ohio Marekani, ni kampuni ambayo iko Marekani na hapa Tanzania.
Hata hivyo kwa mara ya kwanza hii kampuni August 30 2013 itamkutanisha bondia Francis Cheka na Mmarekani Derrick atakaekua bondia wa kwanza Mmarekani kuja kupigana Tanzania.
Siku hiyohiyo ya August 30 pia mabondia Mada Maugo na Thomas Mashari watashuhudiwa wakizichapa live.
.
.

No comments:

Post a Comment