TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, July 29, 2013

MBONI AFUTURISHA
 
Rais Mstaafu wa Awamu wa Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi akizungumza baada ya futari.
 Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (CCM), Dk. Asha-Rose Migiro (kushoto) naye alikuwa miongoni mwa waalikwa.
Sauda Mwilima (kushoto), mchumba wa Diamond Penny Mungilwa (kati) na dada wa Diamond Hasna (kulia) wakifuturu.
Mwanamuziki  wa miondoko ya mduara Zuwema Mohamed 'Shilole' (wa pili kulia) akiwa na wageni wengine waalikwa.
Baadhi ya wageni waalikwa.
Meya wa Ilala Jerry Slaa (kulia) na wageni wengine wakati wa futari hiyo.
Mkurugenzi  wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' Asha Baraka (kushoto) naye alikuwepo.
Mtangazaji wa kipindi cha Mboni Show, Mboni Masimba akiongea jambo.
Shekhe Sharif (kushoto) naye alikuwepo kwenye futari hiyo.
Mboni akiwa na baba yake mzazi mzee Masimba.
Mboni akifanya mahojiano na Mzee Mwinyi.
Mboni akimkabidhi zawadi ya kikombe Mzee Mwinyi.
Mboni akimuelekeza Mzee Mwinyi sehemu ya kusaini.
Mzee Mwinyi, Mboni pamoja na Asha Rose Migiro wakiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima kutoka vituo mbalimbali.

Penny, Husna na Joan katika pozi.
Kutoka kulia: Shilole, Husna, Penny katika pozi na baadhi ya waalikwa.
MTANGAZAJI wa kipindi cha Mboni Show kinachorushwa kupitia televisheni ya East Afrika, Mboni Masimba jana alifuturisha wageni mbalimbali na viongozi akiwepo Rais Mstaafu  wa Awamu ya Pili, Mhe Ali Hassan Mwinyi na Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (CCM) ambaye pia alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Matifa, Dk. Asha - Rose Migiro, katika ukumbi wa Karimjee uliopo Posta jijni Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment