TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, July 25, 2013

CHINA KUSHIRIKIA​NA NA CCM KATIKA UJENZI WA CHUO CHA IHEMI IRINGA 

IMG 2994 9c1f0Kamanda wa UVCCM mkoa wa Iringa Salim Abri Asas kushoto akiagana na katibu mkuu wa CCM Taifa Abdulrahman Kinana  katika uwanja wa ndege Nduli  mkoani Iringa baada ya kukamilisha ziara ya balozi wa china nchini Bw Lu Youqing kwa ajili ya kuanza ushirikiano na CCM kwenye ujenzi wa chuo cha Ihemi.

SERIKALI ya nchi ya China imekusudia kushirikiana na chama cha mapinduzi (CCM) katika kufufua chuo cha vijana Ihemi katika wilaya ya Iringa mkoani Iringa kwa ajili ya kukiwezesha chuo hicho kutoa mafunzo ya uongozi kwa vijana kutoka nchi za Sadac pamoja na nchi ya China .
Katika kuonyesha mikakati ya awali ya kuanza kukifufua chuo hicho balozi wa chini nchini Tanzania Bw Lu Youqing leo amekitembelea chuo hicho chenye eneo la ukubwa wa hekari 1900 na kuonyesha kuvutiwa zaidi na eneo hilo.
Akielezea mkakati huo katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Taifa Nape Nnauye alisema kuwa CCM inaompango wa kukiendeleza chuo hicho kwa kushirikiano na serikali ya China .
"Leo tumekuja na balozi wa China kwa ajili ya kupaendeleza zaidi ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya uongozi pamoja na masuala ya ujasiriamali ambayo yatawafanya zaidi vijana kuweza kujiajiri zaidi"
Alisema kuwa mpango wa kukifufua chuo hicho unataraji kuanza mara moja na kuwa hayo ni maamuzi ya mkutano mkuu wa Taifa ambayo utekelezaji wake unaanza mara moja .
Nnauye alisema kuwa kutokana na maamuzi hayo ya mkutano mkuu wao wameanza kufanyia kazi suala hilo kwa kuwatafuta wahisani hao kutoka China ambao watasaidia kufanikisha ujenzi huo ambao kukamilika kwake ni ukombozi mkubwa kwa vijana nchini nan chi nyingine .
Pia alisema kuwa kuyumba kwa chuo hicho kunatokana na mfumo wa vyama vingi na kuwa kabla ya mfumo wa vyama vingi kuanza chuo hicho cha Ihemi kilikuwa kikifanya kazi vema japo alisema kwa sasa mkakati ni kukifufua na kuwa chuo hicho kitakamilika ndani ya mwaka huu .
Kuhusu aina ya mafunzo yatakayotolewa alisema kwa sasa ni mapema sana ila mara baada ya ujenzi kukamilika basi aina ya mafunzo yatakayotolewa yatajulikana .
Nnauye alipoulizwa kuhusu gharama ya jumla itakayotumika kujenga chuo hicho alisema kuwa kwa sasa bado ni mapema kujua ni kiasi gani kitatumika katika ujenzi na kuwa hatua iliyopo sasa ni ya awali zaidi .
Katika ziara hiyo ya balozi wa China nchini aliongozana na msaidizi wake Bi.Wang Fang pamoja na katibu mkuu wa CCM Taifa Abdulrahman Kinana ,katibu mkuu wa UVCCM Taifa Martine Shegela pamoja na viongozi mbali mbali wa chama na serikali wilaya na mkoa wa Iringa .

No comments:

Post a Comment