TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, July 22, 2013

Mhe Makamba mgeni rasmi semina ya usalama wa matumizi ya kompyuta 

Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini January Makamba akizungumza na waandishi kuhusu mipango ya kamati yake kuangalia tat
Na:Lorietha Laurence-Maelezo
Taasisi huru isiyo ya kiserikali kutoka nchini Marekani inayoitwa ISACA tawi la Tanzania kwa kushirikiana   na kampuni ya Norway inayoshughulikia maendeleo Afrika Mashariki (Norway Registers Development  East Africa Limited –NRD-) wameandaa semina  ya usalama wa matumizi ya  kompyuta na mitandao yake katika nyanja mbalimbali kwa mashirika ya umma, benki, serikali na watu binafsi.Semina hiyo 
 inayotarajiwa kufanyika Agosti 28 hadi 30  mwaka huu katika Hoteli ya Nashera mkoani Morogoro ambapo Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  Mhe January Makamba anatarajiwa kuwa mgeni rasmi  .
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar Es Salaam Rais wa ISACA Bw. Boniface Kanemba ameeleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu kutokana na   ongezeka la wizi wa mitandao  na matumizi mabaya ya mitandao uliojitokeza katika miaki ya hivi karibuni.
“Mafunzo haya ni kwa ajili ya wadau mbalimbali kutoka sekta zote za umma na binafsi  pia kutoka nchi zote tano za Afrika Mashariki zikiwemo, Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi kutokana na nchi hizi kuwa na changamoto sawa  na ongezeko la wizi wa mitandao “alisema Kanemba.
Rais huyo wa ISACA ameongeza kuwa changamoto kubwa ya wizi wa mitandao inatokana na kuongezeka kwa matumizi ya mitandao ya simu katika kutuma na kupokea pesa.
Hivi karibuni, makampuni ya simu yamekuwa yakitumia mtandao mfano M-pesa na Tigo Pesa kutuma hela kwa wateja ambapo kumekuwa na kesi nyingi za wizi kwa kutumia miamala hiyo pamoja na upotevu wa nyaraka muhimu za makampuni binafsi ,umma na Serikali.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa NRD East Afrika Sebastian Marondo akizungumzia umuhimu wa semina hiyo amesema, “sio jukumu la serikali peka yake kupambana na uhalifu bali ni jukumu la kila mwananchi ,makampuni na mashirika binafsi katika kulinda  na kujenga nchi yetu.”
ISACA ni taasisi huru ya kimataifa   isiyokuwa ya faida  inayohusika  katika kusimamia na kutoa mafunzo na maarifa ya mifumo ya mitandao wakati NRD East Afrika  ni kampuni inayojihusisha na mifumo ya mitandao ya kompyuta na usalama wake.

No comments:

Post a Comment