TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, July 22, 2013

YANGA,URA WATOKA SARE 2-2
yanga2 dce9c
 Mshambuliaji wa URA akijaribu kuwatoka mabeki wa Yanga (HM)
 yanga cc512
MABINGWA wa soka Tanzania bara, klabu ya Yanga angalau jana wamepata cha kusema baada ya kupata sare ya 2-2 dhidi ya Wakusanyaji wa Mapato wa nchini Uganda, klabu ya URA, katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Yanga waliponea chupuchupu kulala kama wenzao Simba siku ya jana ambapo waliburuzwa 2-1 na wakali hao wa Uganda, lakini mshambuliaji ambaye hajaifungia Yanga kwa muda mrefu, Jerryson Tegete aliwapa cha kusema mashabiki wao baada ya kusawazisha bao la pili dakika ya 90 ya kipute hicho.

Afisa habari wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema Yanga walicheza vizuri kipindi cha pili, lakini kipindi cha kwanza URA walitawala zaidi mchezo wakipiga soka la uhakika.
Kizuguto alisema kocha wa klabu hiyo Ernie Brandts amesisitiza kuwa kikosi chake kimecheza vizuri, lakini wapinzani wake walikuwa wazuri sana.
Afisa habari huyo alisema kesho kikosi hicho kitakuwa na mapumziko, na kesho kutwa jumanne kitaendelea na mazoezi yake katika uwanja wa shule ya Sekondari ya Loyola mabibo jijini Dar es salaam.
“Mechi ya leo ilikuwa nzuri sana kwa kikosi chetu, kocha amewapima wachezaji wake mbele ya timu nzuri, lakini sisi bado timu yetu ni nzuri sana”. Alisema Kizuguto.
Pia alisema hamasa ya mashabiki wa Yanga uwanjani imeonesha kuwa wanaipenda timu yao na wanatakiwa kuwa na moyo wa kuipenda zaidi kwani itawapa raha.
“Yanga ni timu ya wananchi,na ndio maana kila inapocheza wananchi wanajitokeza kwa wingi, hakika hatutawaangusha hata kidogo”. Alisema Kizuguto

No comments:

Post a Comment