VIJANA WAASWA
Waziri
 wa Habari Vijana,Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Dk Fenella Mukangara 
akizungumza na washiriki wa kambi ya vijana leo jijini Dar es Salaam 
alipokuwa akifungua rasmi kambi hiyo ambayo imeanza tarehe 29 na 
inatarajiwa kumalizika tarehe 2 Agosti.Kambi hiyo ya vijana ya Dunia 
imeandaliwa na taasisi isiyo ya Kiserikali International Youth 
Fellowship(IYF) kwa kushirikiana na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni 
na Michezo.
Baadhi ya washiriki wa kambi ya vijana
 wakisikiliza hotuba ya Mheshimiwa Waziri Fenella Mukangara hayupo 
pichani alipokuwa akifungua rasmi kambi hiyo leo jijini Dar es Salaam
        
Na Frank Shija - Maelezo
Vijana 
nchini wameaswa kujitambua na kuthubutu kwa malengo chanya pamoja ikiwa 
ni pamoja na kujituma kufanya kazi zikiwemo za kujitolea kwa kuwa kwa 
kufanya hivyo wataweza kujikwamua na kujiletea maendeleo yao na Taifa 
kwa ujumla..
Rai hiyo 
imetolewa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk Fenella 
Mukangara alipokuwa akifungua kambi ya dunia ya vijana leo jijini Dar es
 Salaam.
Waziri 
Fenella amesema kuwa vijana wengi wamekuwa wakiishi kwa mazoe na kufuata
 mikomba ambapo ni hatari sana matokeo yake wamekuwa wakijikuta 
wakitenda tofauti na malengo yao.
Aliongeza
 kuwa ni wakati sasa kwa vijana kujitambua na kubadilisha fikra zao hili
 waweze kujiletea maendeleo wao wenyewe baadala ya kulalamika kama 
ambavyo wamekuwa wakifanya.
"Ni 
muhimu vijina mjitambue na mthubutu kwa malengo chanya, na muanze kwa 
kila mmoja wenu kujituma kufanya kazi na wakati mwingine jitoleeni kwa 
faida ya jamii zenu". Alisema Waziri Fenella
Aliongeza
 kuwa Mungu amewajali vijana Talanta na vipaji tofauti hivyo ni muhimu 
vikatumika kwa ajili ya maendeleo yao wenyewe na Taifa kwa ujumla na 
kuongeza kuwa kujitambua kwa vijana kuendane na uthubutu ili kujikwamu 
kimaendeleo.
Kwa 
upande wake mwanzilishi wa IYF duniani Pastor Park Ock Soo amesema kuwa 
ni faraja kwake kuona vijana wengi wamejitokeza kushiriki kambi hiyo 
akiamini malengo ya kuanzishwa kwa taasisi yake yamefikiwa kwa kiasi 
kikubwa.
Pastor 
Park ameongeza kuwa vijana wanapaswa kubadili fikra na mitazamo yao ili 
kuenenda na kasi ya kujiletea maendeleo badala ya kulalamika na kusubiri
 kufanyiwa kazi.
Kambi hii
 ya vijana ni inafanyika hapa nchini kwa mara ya tano na imeandaliwa na 
taasisi ya International Youth Fellowship (IYF) kutoka Korea kwa 
kushirikiana na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, ambapo 
kauli mbiu ya mwaka huu ni "Badilisha Fikra ktuoka mtazomo hasi kuw 
chanya"
No comments:
Post a Comment