TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, July 30, 2013

MASTAA 10 WA KIKE KUTOKA HOLLYWOOD WALIOLIPWA MAMILION YA DOLA ZAIDI YA MASTAA WENGINE WOTE KWA MWAKA 2012-2013

hollywood-sign
Nani analipwa pesa nyingi kwa movie anazofanya?, swali hili limeleta utata mara kadhaa pale mastaa wengi wa bongomovie wanapoulizwa na vyombo vya habari na kushindwa kujua hadi leo msanii yupi analipwa pesa nyingi kwa movie anazocheza. Lakini ukija kwenye anga za Hollywood, sio siri hata kidogo kuhusiana na nani kavuna pesa nyingi mwaka huu kwenye kazi za uigizaji. Kitu hiki pia kinasaidia kuongeza thamani na hata uhitaji wa movie producer na directors wengi kutaka kupanga waigizaji hawa kwenye movie zao kwasababu ya image wanayoipata  kwa jamii baada ya kujulikana kuwa wanaolipwa pesa nyingi kwenye uchezaji wa movie zao. Bongomovie siku moja itakuwa nzuri ikiwa tukijua hata kwa mwaka mmoja uliopita nani kavuna pesa nyingi kwenye kazi za uigizaji.
Hii hapa ndiyo list ya waigizaji wa kike huko Hollywood walivuna pesa nyingi sana kuanzia June 2012 hadi June 2013.
World War Z - World Premiere - Red Carpet Arrivals
Angeline Jolie – $33 million
Mkali wa movie kama Mr and Mrs Smith,Tom Rider, Tourist na nyingine nyingi mara kadhaa amehusishwa kwenye mdahalo wa kwanini Angeline Jolie ni most powerful woman in Hollywood. Hii list inaendelea ku-prove ukweli juu ya sentensi hii, Angelina Jolie ambaye pia ameanza kujihusisha na maswala ku-direct movie ameingiza kiasi cha dola millioni 33 katika kipindi cha miezi 12. Angeline ana miaka 38 na watoto sita ikiwa wengine ni wa ku-adopt.
'Jimmy P. (Psychotherapy Of A Plains Indian)' Premiere - The 66th Annual Cannes Film Festival
Jennifer Lawrence- $26 million
Mshindi wa tuzo kubwa na zenye heshima kwenye movie industry huko Hollywood, hapa nazungumzia Oscar Awards ambazo mastaa wengi wanatamani kuzipata lakini yeye ameipata kama muigizaji bora wa kike akiwa na miaka 22 tu. Unaambiwa hadi jarida la Times walimuweka kwenye list ya 1oo most influential people duniani.Profile hii ni kubwa sana, kuna kipi cha kumzuia asiwe kati ya waigizaji wanaolipwa pesa nyingi huko Hollywood. Young,talented and still getting it kwenye bank account.
85th Annual Academy Awards - Arrivals
Kristen Stewart – $22 million
Watu wangu wa The Twilight mtakuwa mnamsoma huyu actress, kati ya mastaa wakubwa watatu wa movie za Twilight na yeye ndiyo msichana pekee. Mwaka jana alikuwa ndio actress anayelipwa ziadi kuliko wote huko Hollywood, mwaka huu amekuwa watatu kitu ambacho sio kibaya.
"Just Go With It" New York Premiere - Outside Arrivals
Jennifer Aniston – $20 million
Licha ya kupata mkwanja mwingine kupitia bidhaa zake kama mineral water na vipodozi vingine, Jennifer Aston bado anakamata nafasi ya pili katika hii list. Pia media zinampenda sana kama Wema huku Bongo, huwa haishiwi story  za kuandikwa. Mwaka 2012 vyombo vingi vya habari viliandika kuhusu kuvishwa kwake pete na actor Justin Theroux
Emma Stone Sighting In New York City - May 28, 2013
Emma Stone – $16 million
Kama ulishawahi kuangalia Amazing Spiderman, yule girlfriend wa spiderman ndiyo huyu Emma Stone. Amazing spiderman ni moja kati ya movie zenye bajeti kubwa alizowahi kufanya, so kwanini asilipwe pesa nyingi kama anafanya movie zenye bajeti kubwa kama Amazing Spiderman.
17th Annual Critics Choice Movie Awards - Arrivals
Charlize Theron – $15 million
Mwaka 2011 alifanya movie kama Young Adult,2012 alifanya movie maarufu ya Snow White and the Huntsman. Charlie Theron anakamata namba 6 kwa kuingiza dola millioni 15.
7
Sandra Bullock – $14 million
Mshindi mwingine wa Oscar,ameingiza dola za kimarekani millioni 14. Yupo namba saba kwenye list ya actress wanaolipwa zaidi huo Hollywood.
Natalie Portman
Natalie Portman – $14 million
Star Wars films, Thor zote hizi anahusika nazo. Kitu kingine ni kwamba Natalie ni mshindi wa tuzo za Oscar, hii ni sababu ya msingi sana ya kufanikiwa kupata kazi kubwa za kumuigizia pesa nyingi.
Oz: The Great And Powerful - UK Premiere - Red Carpet Arrivals
Mila Kunis – $11 million
Mwanamke ambaye pia anatajwa kati ya wanawake warembo huko Hollywood , mwaka huu ameingia kwenye hii list kutokana na movie kubwa kama TED najua hii  wengi mnaijua kutoka na kuwa maarufu sana. Pia movie kama Oz: The Great and Powerfulearned  ambazo kwa pamoja zimefanya vizuri na kuingiza dola za kimarekani zaidi ya billioni moja. Mila Kunis pia alifanya vizuri kwenye movie ya Friends with Benefit akiwa na Justin Timberlake ambayo pia ni moja kati ya movie zake maarufu miaka iliyopita.
Julia Roberts
Julia ROberts – $11 million
Julia ni actress ambaye anachagua sana movie za kufanya, lakini hiyo sio sababu ya kumfanya asiwe kwenye hii list. Licha ya kuchagua hizo movie, yeye ndiyo anatufungia list hii kwa kuwa na dola millioni 11.

No comments:

Post a Comment