TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, July 31, 2013

MKOA WA RUKWA KUJENGA CHUO KIKUU

IMG 1295 c867c
Jennifer Chamila-Maelezo
MKOA wa Rukwa unatarajia kuanzisha chuo kikuu ambacho kitasaidia vijana wengi wanaokosa nafasi za kuendelea na elimu ya juu kwa kupata nafasi ya kujiunga na chuo kikuu.
Mkakati huo unaosimamiwa na Jukwaa la Maendeleo Mkoa wa Rukwa(JUMARU) ambao ni halali chini ya sheria za nchi ilioanzishwa mwaka 2009 na wakazi wa mkoa wa Rukwa(Wanarukwa) kwa lengo la kuunganisha nguvu za wanarukwa wote ili kuleta maendeleo katika mkoa huo na wakazi wake.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Sekretariati wa JUMARU Bw.Joachim Sikulumbwe amesema kuwa wameandaa kongamano la wanarukwa wote waishio jijini Dar es Salaam litakalo fanyika Septemba 01 mwaka huu,katika ukumbi wa Ubungo –Urafiki Social hall.
"Kongamano hilo litazungumzia maliasili na rasilimali za mkoa wa Rukwa na maendelao yake ,kiuchumi,kisiasa,kijamii na kiutamaduni nawaomba wanarukwa wajitokeze na kuhudhuria kwa wingi"alisema bw. Sikulumbwe,
Naye Makamo mwenyekiti kamati ya wahadhiri mchakato wa chuo kikuu cha Rukwa bw.Bernard Kasimila amesema sababu ya kuanzisha chuo hicho ni kuwezesha vijana wenye sifa za kuendelea na masomo kupata fursa ya kujiunga na chuo kikuu.
Mkoa wa Rukwa ni sehemu ya Tanzania iliyoko nyanda za juu kusini yenye wakazi zaidi yawakazi milioni moja kwa sense ya 2012 , una wilaya 3, halmashauri 4,tarafa 17,kata 64,na vijiji 202,unajishughuli zaidi na kilimo,uvuvi na utalii.
Mwisho

No comments:

Post a Comment