TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, July 31, 2013

ASHTON : MOHAMMED MORSI YUKO SALAMA 

050 71c67MWAKILISHI wa mambo ya nje katika Muungano wa Ulaya Catherine Ashton amekutana na Rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri Mohammed Morsi katika eneo lisilojulikana. Morsi amekuwa akizuiliwa na jeshi tangu kuondolewa madarakani mapema mwezi huu.
Ashton amewaambia waandishi wa habari mjini Cairo kwamba Bw. Morsi alikua salama na kwamba alikubaliwa kutazama habari kwenye runinga na kusoma gazeti.
Alisema walijadili haja ya Misri kuganga yajayo na kuweka amani.Baroness Ashton amesema mchakato wa utawala mpya sharti ushirikishe pande zote. (HM)
Msemaji wa Bi Catherene Ashton, alisema kuwa mkutano ulifanyika katika eneo lisilojulikana ambako Morsi anazuiliwa na kuwa ulidumu kwa masaa mawili.
Hakutoa maelezo kuhusu walichokijadili.
Hata hivyo tayari ameshakutana na maafisa kadhaa wa serikali akiwemo rais wa muda Adly Mansour, mkuu wa majeshi, Generali Abdel-Fattah al-Sisi na makamu wa rais wa maswala ya kigeni,Mohamed ElBaradei.
Alisema kuwa atatoa wito kwa pande zote mbili kushirikishwa katika serikali. Ziara ya Ashton ambayo ni ya pili nchini Misri inakuja baada ya wafuasi zaidi ya sabini wa Morsi kuuawa kwenye makabiliano na vikosi vya usalama nchini Misri.
Wafuasi wa kiongozi huyo wamesema kuwa wanapanga kufanya maandamano Jumanne huku serikali ya muda ikiwatahadharisha dhidi ya kuhusika na ghasia na kuwa watakaovunja sheria watachukuliwa hatua.
Maafisa wa usalama pia wametishia kuvunja maandamano ya wafuasi hao waliopiga kambi nje ya medani iliyo karibu na msikiti wa Rabaa al-Adawiya mjini Cairo. Chanzo: bbcswahili

No comments:

Post a Comment