TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, July 18, 2013

BALAZA KUU LA USALAMA UN LAJADILI USALAMA WA WAANDISHI
556660 - Copy b825cBw. Richard Engel kutoka NBC News mmoja kati ya waandishi wanne walioalikwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kueelezea uzoefu wao na mikikimikiki wanayokumbana nayo wanapotekeleza majukumu yao ya kiuandishi. Bw. Engel ambaye amesema amewahi kutekwa, alilitaka Baraza Kuu la Usalama linapojadiliana kuhusu dhana nzima ya usalama wa waandishi, kujadili pia ni nani hasa mwandishi wa habari anaye stahili ulinzi na akahoji kama wanaharakati ambao nao wanachukua picha za matukio mbalimbali na kuzipost kwenye blog kama nao ni waandishi wa habari. pembeni yake ni Bi. Kathleen Carroll, ambaye ni mhariri mtendaji wa Associated Press na Makamu mwenyekiti wa Bodi ya Kamati ya Kulinda Waandishi ( CPJ) yeye katika mchango wake alisema licha ya kwamba waandishi wengi wanapoteza maisha wakati wakitafuta habari kwenye maeneo yenye migogoro lakini waandishi watano kati ya sita wanauawa ndani ya nchi zao wakati wakitimiza majukumu yao.

No comments:

Post a Comment