TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, July 25, 2013

TAIFA STARS YAWASILI KAMPALA KUIKABILI THE CRANES

031 74361
 Wachezaji wa Stars wakitua Kampala (HM)
032 a6685
TIMU ya Taifa (Taifa Stars) imewasili Uganda jana jioni tayari kuikabili Uganda Cranes kwa mechi ya marudiano kutafuta tiketi ya kucheza katika mashindano ya CHAN.
Kikosi hicho chichi nye wachezaji 20, kiliwasili muda mfupi baada ya saa kumi alasiri huku wachezaji na benchi la ufundi wakiwa na matumaini makubwa.
Akiongea mara baada ya kuwasili Kocha wa Timu ya Taifa Kim Poulsen alisema wamejiandaa vizuri wakiwa
Mwanza na ana imanikikosi hiki kitabadili matokeo ya awali ambapo Stars ilifungwa 1-0 na Cranes Jijini Dar es Salaam.
Alisema licha ya kuwakosa wachezaji Shomari kapombe na Mwinyi Kazimoto, ana imani na kikosi chake hiki kuwa kitafanya makubwa Kampala.
 “Tumekuja kubadilisha mahesabu kwani tumejiandaa vizuri kabisa,” alisema Poulsen.
Wadhamini wa Stars, Kilimanjaro Premium Lager wamewaomba watanzania wasikate tama kwani Stars bado ina nafasi kubwa ya kupindua meza.
 
“Sisi kama wadhamini bado tuna imani na Stars na tunajua watatuwakilisha vizuri ni vyema watanzania wawe na imani na kuiombea dua timu iibuke na ushindi mnono katika mechi hii ya marudiano,” alisema Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, george Kavishe.
Mechi hii ni gumzo kubwa Jijini Kampala kwani baadhi ya waganda wana hofu kuwa henda wakafungwa nyumbani kwao.
Mechi hii itapigwa katika Uwanja wa Nambole Jijini Kampala JUmamosi hii saa kumi jioni.
Mashindano ya CHAN yanatarajiwa kufanyika Januari mwakani nchini Afrika Kusini

No comments:

Post a Comment