PSG BIGWA UFARANSA BECKHAM AWEKA REKODI

David Beckham na Zlatan Ibrahimovic wakishangilia kuiwezesha PSG kutwaa taji la kwanza baada ya miaka 19.

Beckham akipongezana na Carlo Ancelotti, kocha wa PSG

Ibrahimovic

Beckham akikumbatiana na mmiliki wa Qatari TV, chaneli ya Al Jazeera Sport ambaye pia ni mmiliki wa PSG, Nasser Al-Khelaif
KIUNGO wa David Beckham ameweka rekodi
ya kutwaa mataji ya Ligi Kuu na klabu za nchi nne tofauti, baada ya PSG
kuifunga Lyon 1-0 na kutwaa ubingwa wa Ligue 1, Ufaransa.
Beckham, ambaye sasa anakuwa mchezaji
wa kwanza wa England kutwaa mataji katika nchi nne tofauti, aliingia
akitokea benchi, wakati Jeremy Menez alipokifungia bao pekee la ushindi
kikosi cha Carlo Ancelotti.
Ubingwa wa PSG hautathibitishwa hadi
Kamati ya Nidhamu ya Ligi itakapokutana kuamua kuipokonya pointi au la
kufuatia tuhuma za Mkurugenzi wake, Leonardo kumrubuni refa. Chanzo:
sportmail
No comments:
Post a Comment