TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, May 19, 2013

MAREKANI INAWASIWASI KUHUSU NIGERIA
 us ab960Wakati wanajeshi wa Nigeria wanaendelea na operesheni yao dhidi ya wapiganaji wa Kiislamu kaskazini mashariki mwa nchi, Marekani imesema ina wasiswasi sana kuhusu raia katika eneo hilo.
Katika taarifa ya Waziri wa Mashauri ya Nchi za Nje wa Marekani, John Kerry, amesema ana wasiwasi kuhusu madai ya kuaminika kuwa wanajeshi wa Nigeria wamekiuka vibaya haki za binadamu.
Bwana Kerry alisema hayo yatazidisha ghasia na kuchochea msimamo mkali.
Nigeria inafanya mashambulio dhidi ya kundi la wapiganaji wa Kiislamu, Boko Haram, katika majimbo matatu ya kaskazini-mashariki. Chanzo: www.voaswahili.com

No comments:

Post a Comment