TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, May 23, 2013

RAIS REAL MADRID AMPELEKA RONALDO CHELSEA
ronaldo2 d17fd
 Ronaldo
 ronaldo 72075
Ronaldo akiwa na Mourinho

RAIS wa zamani wa Real Madrid, Ramon Calderon amekuza matumaini ya Cristiano Ronaldo kufuatana na Jose Mourinho Chelsea... baada ya kupuuza nafasi ya Manchester United kumsajili tena nyota huyo Mreno.
Ronaldo, mwenye umri wa miaka 27, yuko kwenye kinyang'anyiro cha kununuliwa kwa Pauni Milioni 80, baada ya kuchoshwa na maisha katika Jiji la Hispania.

Alipoulizwa kama 'kipepeo' huyo wa Ureno alikuwa ana furaha Real Madrid, Calderon alisema: "Ronaldo amesema alikuwa ana machungu mwanzoni mwa msimu. Nafikiri uhusiano wake na rais wa sasa si mzuri, labda kwa sababu rais hapendi wachezaji aliowakuta.

"Si timu nyingi zinazoweza kumlipa kile anachostahili na pia itakayoweza kuilipa Real Madrid kile wanachotaka. Kuna klabu tatu - Manchester City, PSG na Chelsea. Sifikiri klabu yoyote nyingine inaweza kulipa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya mchezaji".

"Wao (Real) wanakwenda kujadili mkataba sasa na watafanya uamuzi. Ni kitu ambacho kitajulikabna ndani ya wiki chache,"alisema.United ina nafasi ya kwanza ya kumsajili Ronaldo ikiwa Real itaamua kumuuza nyota huyo wa Ureno itampa kipaumbele cha kurejea Old Trafford. Chanzo: binzubeiry

No comments:

Post a Comment