TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, May 30, 2013

"SIELEWI MSINGI WA KAULI YA SITTA "JOHN MAGUFULI
d1 e3e51

Kauli ya Magufuli
Akizungumza na gazeti hili nje ya ukumbi wa Bunge jana, Dk Magufuli alisema haelewi msingi wa kauli ya waziri mwenzake huyo, kwani hajui chochote katika mtandao wa urais alioutaja.
Magufuli alisisitiza kusema hana kundi, hakuwahi kuzungumza wala kuhudhuria vikao vya kundi lolote, na kwamba kundi lake ni CCM na Mwenyekiti wake ni Jakaya Kikwete.
“Sina kundi. Sijawahi kuwa na kundi na sitarajii kuwa na kundi lolote. Ninachojua kundi langu ni CCM na kiongozi wake ni mwenyekiti wake, Rais Kikwete,” alisema Dk Magufuli.
Hata hivyo, Dk Magufuli pia alipuuza taarifa kuwa alichangia harambee hiyo akisema, “Si kweli, Mwanza sijatoa hata senti na hata siku ilipofanyika hafla hiyo, nilikuwa Dar es Salaam katika mkutano na makandarasi.” Licha ya kutajwa kuwa miongoni mwa vinara wa urais 2015, Magufuli alieleza kuwa hakuwahi kuzungumza na Sitta suala hilo linalohusu makundi ya urais mwaka 2015.
Sitta azungumza
Akizungumza na gazeti hili baadaye jana, Sitta alikiri kuwa hawakuwahi kuzungumzia suala la kuwania urais isipokuwa ni hisia zinazojengwa na kuwa majina yanatajwa kuwa wanautaka urais.
“Nilishasema kuwa umoja wetu tuliouunda ni wenye sauti sawa ni kupigania hali za wananchi wanyonge, na hata kwenye mikutano yetu ya ndani tunasema sisi ni dhidi ya watu wanaokwenda kinyume na maisha ya wanyonge.
“Na ni kweli nilitamka kuwa katika umoja wetu, ikiwa itaonekana mmoja wetu anafaa na watu wakataka awanie urais, basi itakuwa hivyo.” CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment