TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, May 30, 2013

WATU 92 WAFIKISHWA MAHAKAMANI MTWARA KUHUSIANA NA VURUGU ZA GESI


Watu 92 wamefikishwa katika Mahakama ya Mkoa wa Mtwara na kusomewa mashitaka mbalimbali, ikiwamo kufanya fujo, kuvunja nyumba, kuiba, kujeruhi na kuhujumu uchumi katika vurugu zilizotekea mjini Mtwara, Mei 22, mwaka huu.

Watu hao walifikishwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Mussa Esanju.
Waendesha Mashitaka wa Serikali, Justine Sanga, na Renatus Mkude, walidai kuwa washitakiwa hao walitenda makosa hayo katika tarehe hiyo. 

Watuhumiwa kwa pamoja walikana mashitaka hayo na kurudishwa rumande.
Uamuzi huo unatokana na wengi wa washtakiwa kukabiliwa na tuhuma za kuhujumu uchumi, kosa ambalo mahakama hiyo haina uwezo wa kuwaachia kwa dhamana.
Hakimu Esanju aliiahirisha kesi hiyo hadi Juni 10, mwaka huu, kwa ajili ya kutajwa.

HABARI  IMEANDIKWA  KWA  KIREFU KATIKA  GAZETI LA NIPASHE

No comments:

Post a Comment