TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, May 26, 2013

BAYERN BINGWA ULAYA YAICHAPA DORTMUND 2-1
soka0 e04ad
Bayern
soka00 7b1e1
Mabingwa wa Ulaya, Bayern
Wajerumani si mchezo katika soka,  fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya  imepigwa katika dimba la Wembley jijini London usiku wa kuamkia leo ambapo kwa mara ya kwanza timu mbili kutoka Ujerumani zimekutana katika mechi kali na ya kusisimua baina ya wekundu wa kusini mwa ujerumani Bayern Munich na nyuki wa kaskazini mashariki mwa nchi hiyo Borrusia Dortmund.

Kwa kawaida mechi nyingi za fainali huwa zinapigwa mpaka dakika 120 mpaka mikwaju ya penati kama ilivyokuwa kwa mwaka jana ambapo Chelsea waliifunga Bayern, lakini fainali ya leo imepigwa ndani ya dakika tisini.
Winga wa FC Bayern Mholanzi Arjen Robben ameipatia klabu yake zawadi kubwa sana ya kutwaa ubingwa msimu huu baada ya kufunga bao la pili na la ushindi katika dakika ya 88 ya kipindi cha lala salama.
Bao hilo limetokana na kazi nzuri ya winga mwenye kasi zaidi Frank Ribery aliyempa pasi nzuri Robben na kupachika bao kiufundi zaidi.
Ubingwa huo ni wa tano kwa Bayern ambao katika misimu minne wamecheza mechi tatu za fainali bila mafanikio. Chanzo: Baraka Mpenja

No comments:

Post a Comment