TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, May 29, 2013

BENITEZ AWEKA NGUMU CAVANA KUONDOKA NAPOLI
napoli 2f7b2
Cavan kulia
KOCHA mpya wa Napoli, Rafa Benitez anataka kumzuia kuondoka katika klabu hiyo mshambuliaji, Edinson Cavani na atafanya naye mazungumzo mshambuliaji wake nyota huyo kumshawishi abaki kwa mmoja zaidi.

Cavani, mwenye umri wa miaka 26, amekuwa akiwaniwa kwa muda mrefu na Manchester City na ameingia kwenye orodha ya washambuliaji tishio Ulaya kwa kuweza kufunga mabao 29 katika mechi 34 za ligi akiwa na Napoli.
Chelsea pia inamtaka mchezaji huyo mwenye thamani ya Pauni Milioni 50 na anayetaka mshahara wa Pauni 250,000 kwa wiki. Wiki iliyopita, Napoli iliikata maini City katika mpango wa kumtaka Cavani, kwa kuwapa ofa ya Pauni Milioni 60 kwa ajili ya Edin Dzeko.

Rais wa klabu hiyo ya Italia, Aurelio De Laurentiis, ambaye alikuwa hataki kuizungumzia City awali, alisafiri hadi London Jumatatu kufanya mazungumzo Mkurugenzi wa Michezo wa klabu hiyo ya Ligi Kuu England, Riccardo Bigon.
City iko tayari kukubali Pauni Milioni 50 – kati ya hizo, Pauni Milioni 30 ni thamani ya Dzeko na kuongeza Pauni Milioni 20– lakini Napoli inataka Milioni 60 na De Laurentiis anasema ni wakati wa kumalizana aLaurentiis anasema ni wakati wa kumalizana au kuacha.
Benitez alitangazwa kuwa kocha mpya Napoli Jumatatu akipewa mkataba wa miaka miwili. Mspanyola huyo anachukua nafasi ya Walter Mazzarri ambaye anahamia Inter Milan, klabu ya zamani wa Benitez. Chanzo: Binzubeiry

No comments:

Post a Comment