TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, May 20, 2013

MHE. PETER MSIGWA AACHIWA KWA DHAMANA 
msgw1 0e1cc
Msigwa akiwa amebwa juu juu na wanachama wa chadema mara baada ya kuachiwa kwa dhamana 
msgw2 c6bfc


msgw3 535e6
Mamia ya wanachama wa chadema wakiandamana kuonyesha furaha yao ya kuachiwa kwa dhamana mhe: mbunge Peter Msigwa 

msgw4 3cc0d
Msigwa akiongea na wapiga kura wake mara baada ya kuachiwa kwa dhamana.

 Na Said Ng'amilo Iringa
MBUNGE wa Iring mjini Mch. Peter Msigwa (CHADEMA) na wafanyabiashara 75 mapema leo walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya wakikabiliwa na makosa matatu .
Msigwa anakabiliwa na makosa mawili ambapo kosa la kwanza ni la kwake pekee yake na huku kosa la pili likiwahusu washtakiwa wote.
Akisoma mashtaka hayo mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya Godfrey Isaya, mwendesha mashta wa serikali Adolf Maganda alisema Peter Msigwa ambaye ni mshtakiwa namba moja anakabiliwa na shtaka la kushawishi watu kutenda uhalifu ambapo alisema Msigwa alifanya ushawishi huo katika mkutano alioufanya Mei 15 Mwaka huu katika maeneo ya mashinetatu.
Kosa la pili ambalo linawakabili watuhumiwa wote 76 limetajwa kuwa watuhumiwa walifanya mkusanyiko pasipo kibali cha polisi na kusababisha uhalibifu, ambapo alisema Mei 19 Mwaka huu watuhumiwa walikusanyika katika maeneo ya mashine tatu bila kibali.
Akisoma kosa la tatu Maganda alisema linawahusu watuhumiwa namba 2 hadi namba 76, alisema mnamo Mei 19 Mwaka huu watuhumiwa waliharibu kwa makusudi gari lenye namba za usajili SM 9323 mali ya kikosi uokoaji na zimamoto Iringa.
Baada ya kusomewa makosa yao, wakili wa kujitegemea Bazil Mkwata alisema makosa wanayokabiliwa nayo wateja wake yanadhamana na hivyo kuiomba mahakama wateja wake wapewe dhamana.
Akitoa masherti ya dhamana hiyo, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya Godfrey Isaya aliwataka washtakiwa kila mmoja kuwa na mdhamini mmoja anayeaminika ambaye anatakiwa kuwa na shilingi milioni moja na kwamba washtakiwa hao wakipewa dhamana wasijihusishe na uhalifu tena.
Hata hivyo mwendesha mashtaka huyo alisema upelelezi haujakamilika na watuhumiwa 49 wapo nje kwa dhamana baada ya kukidhi masharti ya dhamana, huku washtakiwa 27 wakirudishwa rumande baada ya kukosa dhamana na kesi hiyo itatajwa tena Juni 3 Mwaka huu.
Washtakiwa hao walipandishwa kizimbani siku moja baada ya kukamatwa katika purukushani za askari kuzuia wafanyabiashara ndogondogo (Machinga) kufanya biashara zao katika maneo ya mashinetatu.
Aidha Katika mkutano wa kiserikali uliofanyika 19 Mei Mwaka huu katika maeneo ya Mashinetatu Msigwa alisisitiza Machinga kutoondoka katika maeneo hayo ili waweze kufanya biashara kwa ajili ya kupata chochote kwa ajili ya familia zao.
Mara baada ya kutoka mahakamani wafanyabiashara na wananchi walimbeba mbunge wao hadi ofisi ya chama iliyopo Mshindo ambako aliongea na wnanchi.
Akiongea na umati wa wananchi Msigwa aliwashukuru wananchi kwa ushirikiano walio uonesha kwake na kwa wafanyabiashara tangu mwanzo wa tukio hadi mwisho, kwa kile alichosema wameonesha uzalendo wa dhati.
"Ninawashukuru sana wananchi kwa uzalendo wenu japo kuwa kuna watu wangu wamekosa dhamana lakini nawaahidi kuwa kesho (leo) nitafanya jitihada zote kwa kushirikiana na viongozi wenzangu kuwatoa. Ila niwatoe wasiwasi kuwa waliobaki watatoka" alisema Msigwa.
Kwa upande wao wafanyabiashara wamemfananisha Msigwa na Mwalimu Nyerere kwa moyo wake wa dhati na upendo wa kweli kwa kile walichosema kuwa anachokisema ndicho anachofanya.
MWISHO.

No comments:

Post a Comment