TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, May 23, 2014

Waziri ajiua kwa kushindwa uchaguzi 

Kabla ya kujiua, aliacha ujumbe kwamba amechukua hatua hiyo baada ya kutokea migongano ya kisiasa.
Wakati Rais wa Malawi, Joyce Banda akizidi kuelemewa kwenye uchaguzi uliofanyika Jumanne wiki hii, Naibu Waziri wa Serikali za Mitaa, Godfrey Kamanya amejiua baada ya kubaini ameshindwa kutetea kiti chake cha ubunge.
Kamanya alijipiga risasi nyumbani kwake mjini Lilongwe saa 9:30 asubuhi baada ya kupewa taarifa hizo kwa ujumbe mfupi wa simu.
Kabla ya kujiua, aliacha ujumbe kwamba amechukua hatua hiyo baada ya kutokea migongano ya kisiasa.
Kamanya aligombea ubunge katika Jimbo la Nzonzi Kusini kupitia People's Party (PP) na mwili wake ulikutwa chumbani kwake na ulipelekewa kuhifadhiwa kwenye Hospitali Kuu ya Kamuzu.(P.T)
Taarifa nyingine zinaeleza kwamba waziri huyo alijiua kutokana na vitisho kutoka kwa mtu asiyefahamika.
Katika matokeo yasiyo rasmi kutoka kituo cha kuhesabia kura cha Lilongwe yaliyotolewa Jumatano asubuhi, mgombea huyo alikuwa ameshika nafasi ya tano kati ya wagombea saba waliowania ubunge kwenye jimbo hilo.
Katika matokeo hayo ya awali, Kamanya alipata kura 1,738 huku mgombea wa Malawi Congress Party (MCP), Higton Jiya akiongoza kwa kura 4,625.
Wakati tukio hilo likitokea, mke wa Kamanya alimpigia simu waziri wa zamani wa usafirishaji, Ulemu Chilapondwa ambaye alikuwa rafiki ya mumewe na kumweleza kuwa amesikia mlio chumbani wakati mlango umefungwa.
Kutokana na taarifa hiyo, Chilapondwa alipofika nyumbani kwa marehemu akiwa na watu wengine wawili walivunja mlango na kukuta mwanasiasa huyo ameshaaga dunia baada ya kujipiga risasi kifuani.
Tukio hilo limekuja wakati mgombea urais kupitia chama chake, Rais Joyce Banda akiwa katika nafasi ya pili akiwa na asilimia 22 ya kura akigongana na Lazarous Chakwera wa Malawi Congress Party (MCP). Anayeongoza ni mgombea urais kupitia Democratic Progressive (DPP), Peter Mutharika kwa zaidi ya asimilia 30.
Chanzo:Mwananchi

No comments:

Post a Comment