Maombi ya mikopo elimu ya juu 2014/2015 yafunguliwa

Mkurugenzi wa Habari,Elimu na Mawasiliano wa HESLB,Cosmas Mwaisobwa
Bodi ya 
Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imefungua maombi ya mikopo 
kwa wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga na Taasisi za Elimu ya Juu 
zinazotambulika kwa masomo ya shahada mbalimbali kwa mwaka wa masomo 
2014/2015.
Akizungumza
 na waandishi wa habari katika ofisi za HESLB jijini Dar es Salaam jana,
 Mkurugenzi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa HESLB, Cosmas Mwaisobwa, 
alisema maombi ya mikopo ambayo yanafanyika kwa njia ya mtandao (Olas) 
yamefunguliwa kuanzia Aprili 23 na yatafungwa rasmi Juni 30, mwaka huu.
Mwaisobwa
 alisema kuwa Bodi inatarajia kupokea maombi ya mikopo kutoka kwa 
waombaji wenye sifa zilizoainishwa kwenye mwongozo na vigezo vya utoaji 
mikopo kwa mwaka wa masomo 2014/2015 ambao ulitolewa na Bodi na 
kutangazwa kupitia magazeti na tovuti yake mwanzoni mwa Aprili, 2014.
Mwongozo 
huo unataja sifa za msingi za waombaji mikopo kuwa wawe ni wahitimu wa 
kidato cha sita, Stashahda na cheti cha elimu ya ufundi ((Tvet) hatua ya
 sita, waliohitimu masomo yao kati ya mwaka 2012 na mwaka 2014 
wanaotarajia kujiunga na elimu ya juu na wanaotarajia kuomba mikopo toka
 Bodi ya Mikopo wanafahamishwa kuwa wanapaswa kutuma maombi yao ndani ya
 kipindi kilichotajwa hapo juu.
Bodi 
inatarajia kutoa mikopo kwa wanafunzi takriban 35,000 wa mwaka wa kwanza
 watakaodahiliwa kujiunga na masomo katika vyuo mbalimbali vya elimu ya 
juu.
"Pamoja 
na kupewa fursa ya kuomba mikopo, waombaji wa mikopo wanapaswa 
kuzingatia masuala ya msingi yanayoambatana na mchakato mzima ikiwa ni 
pamoja na kusoma kwa umakini mwongozo na vigezo vya utoaji mikopo kwa 
mwaka wa masomo 2014/2015 kabla ya kulipa ada ya maombi na kujaza fomu, 
kusoma kwa umakini na kujaza vipengele vyote vya fomu kulingana na 
maelekezo ili kuiwezesha Bodi kupata taarifa sahihi za mwombaji," 
alifafanua Mwaisobwa.
Aliongeza
 kuwa ni muhimu kwa mwombaji mkopo kuambatanisha nyaraka zinazohitajika 
kama vile cheti cha kuzaliwa, vyeti vya taaluma, vielelezo vya mdhamini 
na uthibitisho wa nyaraka kutoka kwa mamlaka husika na mwisho kutuma 
fomu kamili na viambatanisho kwenye Bodi ya Mikopo ili ziweze kupitia 
kwenye mchakato wa uchambuzi na upangaji wa mikopo kwa wakati.
Aidha, 
Mwaisobwa alieleza kuwa kuna mabadiliko machache yamefanyika ambapo 
wanufaika wa mikopo wanaoendelea na masomo hawatakiwi kujaza tena fomu 
kuthibitisha uhitaji wao wa mikopo kwa mwaka unaofuatia. CHANZO: NIPASHE (FS)
No comments:
Post a Comment