TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, May 5, 2014

Wajumbe wa Baraza la usalama wataka uwajibikaji kwa mzozo Sudan Kusini 


Baadhi ya watoto huko Sudan Kusini mustakhbali wao uko mashakani kutokana na mapigano yanayoendelea nchini mwao. (Picha: UNMISS/Tina Turyagyenda.
Wajumbe wa baraza la usalama waliopatiwa fursa ya kuchangia hoja baada ya kuwasilishwa kwa ripoti kuhusu hali ya haki za binadamu Sudan Kusini wamesema kinachoendelea hakikubaliki na ni aibu kubwa.
Mapigano ya wenyewe kwa wenyewe Sudan Kusini  yalianza tarehe 15 Disemba mwaka jana kati ya vikosi vya serikali na vile vinavyomuunga mkono Makamu Rais wa zamani Riek Machar.
Mmoja wa wajumbe hao ni Mwakilishi wa kudumu wa Rwanda kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Eugene Richard Gasana ambaye amesema matumaini yaliibuka wakati wa uhuru wa Sudan Kusini mwaka 2011..
(Sauti ya Balozi Gasana.)
"Hata hivyo miaka mitatu baadaye na kwa kuzingatia kuenea kwa mauaji ya raia pamoja na hali ya haki za binadamu kama ilivyoelezwa na watoa ripoti wa leo na pia kusisitizwa na Balozi Samantha, hatuwezi kubakia watazamaji tu. Huwezi kugombania uhuru kwa miaka na baadaye kugeuka na kuanza kuua raia wako wewe mwenyewe. Ni aibu!"
Mwakilishi wa Kudumu wa Uingereza Balozi  Mark Lyall Grant akasema ripoti za Bi. Navi Pillay na Adama  Dieng zimeweka dhahiri ukiukwaji wa haki za binadamu na akaunga mkono hatua za Muungano wa Afrika na IGAD za kupatia suluhisho la mapigano yanayoendelea. Balozi akatoa mapendekezo. (CHANZO:UM REDIO) (FS)

No comments:

Post a Comment