TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, May 23, 2014

Kupima Virusi vya Ukimwi ni jambo la hiari 

taaaaaaaaaa_d82f0.jpg

Na Ali Issa Maelezo -Zanzibar

Kupima Virusi vya Ukimwi linabaki kuwa  jambo la hiari  kwa muhusika na linaweza kuwa ni kitu cha lazima iwapo  Daktari au Mahakama wamefikia maamuzi ya  kufanya hivyo kwa  sababu maalum ya  kupatiwa ufafanuzi  wa  jambo. (FS)

Hayo yamesemwa jana huko Baraza la Wawakilishi  Mbweni, nje kidogo ya mji wa Zanzibar na Waziri wa Nchi Ofisi ya Mkamu wa Kwanza wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji wakati akijibu suali la Mwakilishi   Jaku Hashimu Ayoub alieitaka  Serikali kuwalazimisha  wananchi  kupima virusi vya ukimwi  kwa kuanzia viongozi wa Serikali na Wanasiasa.

Alisema  Zanzibar ni Sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo imeridhia mikataba ya Kimatafa na Kikanda  na kuheshimu haki za Binadamu, hivyo Zanzibar inawajibu wa kuzingatia na kutekeleza kwa vitendo maazimio ya Ulimwengu ambayo yanakataza kuwalazimisha watu kupima ukimwi.

 “Muongozo wa Shirika la Kazi Duniani juu ya masuala ya ukimwi ni sehemu za kazi  na linapinga kuwalazimisha watu kupima virusi vya ukimwi hasa  wanapotaka kuomba kazi au shurutisho kwa waajiriwa,”alisema Waziri Fatma.

Aidha Waziri huyo alisema kua kushurutisha upimaji wa virusi vya ukimwi ni njia mojawapo ya kuwanyanyapaa na kuwabagua watu waishio na  hivyo na hilo pia ni kinyume na sera za nchi na Mikataba ya Kimataafa dhidi ya ugaguzi.

Hata hivyo Waziri  wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais alisema sera ya Taifa ya 2006 imeweka miongozo tosha ya upimaji virusi vya ukimwi kwa lazima pale ambapo Mahakama na Hospitali  zitalazimika kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria.

“Hatua hii itafanyika iwapo  pametokea udhalilishaji wa kijinsia na ubakaji, naomba nisisitize kwamba suala la ajira, nafasi za uongozi wa kisiasa na Serikali halikuwekewa ulazima wa kuchunguza virusi vya ukimwi,” aliongeza Waziri.

Pamoja na hayo Waziri Fatma alisema Baraza la Wawakilishi lilipitisha mswada wa sheria  desemba 2013 wa  kuweka masharti  ya kukinga na kusimamia masuala ya ukimwi  Zanzibar kulinda na kuheshimu haki za watu wanaoishi na virusi vya ukimwi..

Waziri huyo alisema hivi sasa ziko baadhi ya Skuli zimeanzisha  somo la ukimwi zikiwa na lengo la kuwajengea wanafunzi  uelewa zaidi wa tatizo hilo ili kuweza kujikinga nalo

No comments:

Post a Comment