TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, May 2, 2014

Timbo la Dhahabu laporomoka Colombia 


Maafisa nchini Colombia bado wanajaribu kuwanusuru takriban watu thelathini waliozikwa wakiwa hai na mamia ya tani ya tope pamoja na mawe baada ya mgodi haramu wa dhahabu kuporomoka usiku wa jumatano. (J M)
Miili mitatu imepatikana lakini maafisa wanasema kuwa udongo uliolewa chepechepe katika eneo hilo umefanya juhudi za uokoaji kuwa ngumu .
Waokoaji wanajaribu kufukua udongo ili kuwanusuru watu waliozikwa .
Takriban mashine saba za kufukua udongo zimekuwa zikihusika katika shughuli ya uokozi katika mgodi huo ulioko kusini magharibi mwa sehemu ya Cauca.
Kando kando mwa mgodi huo wapo mamia ya jamaa na marafiki ya wachimba migodi waliofukiwa ambao wanafuatilia kwa karibu shughuli za uokoaji.
Lakini mmoja wa wazima moto amesema kuwa hamna matumaini makubwa
Huku matumaiani yakizidi kudidmia , Rais wa Colombia, Juan Manuel Santos ameulaumu uchimbaji migodi haramu kwa kusababisha vifo hivyo .
Amesema serikali yake inapigana vita dhidi ya uovu huo.
Lakini mwandishi wa BBC ameongezea kuwa kuna migodi kadhaa katika maeneo fiche nchini humo.
Ijumaa wiki iliyopita, wachimba migodi wengine wanne walipoteza maisha yao huku sitini na tano wengine wakiathirika na gesi ya sumu katika sehemu ya Antioquia
chanzo : BBC

No comments:

Post a Comment