TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, May 18, 2014

JAJI WARIOBA:VIONGOZI WATOA MATUSI WANA MATATIZO YA MAADILI 

w_83730.jpg
"Katika hali ya kawaida kiongozi anatarajiwa kuwa mfano kwa kutenda sawa kimila, kidesturi na kisheria lakini ninashangaa kushuhudia kiongozi akitoa lugha zisizofaa na hata matusi, ni ishara ya mmomonyoko wa maadili kwa kiwango kisichomithilika."
Siyo kauli yangu, ni kauli ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Waziri Mkuu mstaafu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali mstaafu na Jaji Joseph Sinde Warioba, akizungumzia utendaji wa Bunge Maalumu.
Amezungumza hayo kupitia kituo cha televisheni cha ITV, kwenye kipindi cha dakika 45 ambacho hutangazwa mara moja kwa wiki.
Wakati hali ikiwa hivyo, Jaji Warioba anasema haelewi lengo la viongozi wa kisiasa wanaopinga mapendekezo yaliyo kwenye rasimu, yanayotaka Katiba ijayo iwe na mwongozo juu ya maadili ya viongozi.
"Hawataki mambo ya maadili ya viongozi yawe kwenye Katiba, wanataka yabaki kwenye sheria hata Uwazi na Uwajibikaji ambazo zimependekezwa kuwa Tunu za taifa kwakuwa ni msingi wa maadili ya viongozi, zinapingwa," anaeleza Jaji Warioba Ingawa anasema hana tatizo na uamuzi wa kuondoa au kuongeza mambo kwenye rasimu, Jaji Warioba anasema haitakuwa sahihi kuondoa matakwa ya msingi ya wananchi.
Anasema kupitia kukusanya maoni kutoka kwa wananchi, wamebaini malalamiko na matarajio mengi ya wananchi yanatokana na kukosekana msingi wa maadili ya viongozi, kwenye Katiba.
Anasema Watanzania wengi wamekata tamaa kutokana na kukithiri vitendo vya rushwa, huduma duni za kijamii na umaskini akisema ufumbuzi wa hayo ni kudhibiti maadili ya viongozi.
Jaji Warioba anasema wapo wanaopinga hata kuwapo ukomo wa kugombea ubunge, hali anayoamini siyo sahihi.
Rais Jakaya Kikwete, akitoa hotuba siku chache baada ya rasimu kuwasilishwa bungeni, akaagiza pendekezo la ubunge kuwekewa ukomo liangaliwe upya na Bunge Maalumu.
"Jiridhisheni na dhana zilizoingizwa, mtakachoona kinafaa kurekebishwa, kuboreshwa au kufutwa msisite tunataka Katiba bora, tofauti yake itapatikana Katiba isiyotekelezeka na kusababisha ilazimike kubadilishwa muda mfupi baadaye," anaeleza na kuendelea.
"Rasimu ina mambo mengi mapya, yatakayobadili mfumo wa utendaji wa nchi, jiridhisheni neno kwa neno, mstari kwa mstari."
Akatoa mfano wa Ibara ya 128.-(2)(d) ya rasimu, sababu za mtu kukoma kuwa Mbunge (d) ikiwa atashindwa kufanya kazi za mbunge kwa muda wa miezi sita mfululizo, kutokana na maradhi au kizuizi ndani ya gereza. Rais Kikwete anasema tatizo halitakiwi kuwa kizuizini bali kupatikana na hatia. Hata hivyo akasema, "Watu wanasema siyo mimi" Bila kuwataja, akasema watu hao wanasema anachositahili mgonjwa ni huduma.
Hoja hapa ni je, kuna ajira ambayo mwajiriwa asipofanya kazi kwa muda huo, kutokana na sababu yoyote zikiwamo zilizotajwa anabaki kwenye ajira? kama haipo, kwa Mbunge.
Rais anatoa mfano wa Ibara ya 125(2)(a) akitaka Wajumbe waiangalie. Inasema; Mtu hatakuwa na sifa za kugombea ubunge ikiwa, (a) aliwahi kuwa Mbunge kwa vipindi vitatu vya miaka mitano.
"Aliyewahi kuwa mbunge kwa awamu tatu eti hatakuwa mbunge milele, duniani kote hawaweki ukomo kwa ubunge hili likipita, tutakuwa wa kwanza," anaeleza Rais Kikwete.
Rais Kikwete anasema watu hao wanatoa mfano wa USA (nchi ya Marekani) kwamba baadhi ya majimbo yameweka ukomo wa kugombea ubunge, lakini wanasumbuana mahakamani kila mara kwa madai ya haki za binadamu kukiukwa."
Akitoa semina kwa Wajumbe wa Bunge hilo, mtaalamu mbobezi wa sheria nchini Kenya, Seneta wa Busia ya Mashariki, Amos Wako, alisema kujifunza kwa nchi nyingine ni vizuri lakini ni kunakiri kitu bila kuzingatia matakwa ya jamii inayolengwa ni hatari.
Seneta Wako aliyeulizwa maswali 40 na wajumbe 16, hakujibu wali hata moja lililolenga kupata ushauri dhidi ya changamoto za mchakato wa Katiba Mpya, alielezwa wazi kuwa majibu ya changamoto hizo yanatakiwa kutolewa na Watanzania wenyewe.
Jaji Warioba ataka wajumbe waweke kando itikadi zao za kisiasa na makundi mengine, ili watumikia taifa. Anabainisha cha msimamo wao wa kusimamia utaifa.(E.L)

No comments:

Post a Comment