BOSI WA UDA KUJIELEZA BUNGENI

Mgogoro 
wa uwekezaji katika Shirika la Usafirishaji Dar es Salama (Uda) 
umechukua sura mpya baada ya Bunge kuamua Mkurugenzi wa Simon Group 
inayoendesha shirika hilo, Robert Kisena ahojiwe na Kamati ya Kinga, 
Haki na Madaraka ya Bunge kutokana na kuingilia kati madaraka hayo.
Agizo 
hilo lilitolewa na Spika wa Bunge, Anne Makinda alipokuwa akijibu hoja 
iliyotolewa na Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika ambaye alitaka 
tuhuma zilizotolewa na Kisena dhidi ya Bunge na wabunge zijadiliwe kwa 
sababu ameingilia uhuru na kinga za Bunge kwa kuzungumza nje ya Bunge 
masuala ambayo yametolewa maelezo na Serikali bungeni.
        
Hoja ya 
Mnyika ilitokana na taarifa za baadhi ya magazeti yaliyotolewa Mei 19, 
mwaka huu yakimnukuu Kisena akisema kuwa wabunge wa Dar es Salaam 
wamehongwa na mfanyabiashara mmoja na kwamba kampuni yake inamiliki hisa
 nyingi tofauti na majibu ya Serikali bungeni.
Akinukuu 
majibu ya Serikali katika swali lililoulizwa na Mbunge wa Kawe (Chadema)
 Halima Mdee, Mnyika alisema kuwa Serikali ililieleza Bunge kuwa 
mgawanyo halali wa hisa za Uda upo kama ulivyosajiliwa kwa msajili wa 
mashirika ya umma, kwamba shirika hilo linamilikiwa na Serikali na 
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.
Katika 
kujenga hoja yake Mnyika alisema majibu hayo yalionyesha kuwa Uda ni 
Shirika la Umma, jambo ambalo lilipingwa na Kisena kupitia mkutano wake 
na waandishi wa habari, akisema Uda inamilikiwa na kampuni yake kwa 
asilimia 76.
Alisema 
kuwa mwekezaji huyo ameingilia haki, kinga na madaraka ya Bunge kinyume 
na utaratibu na kuanza kuwatuhumu wabunge ambao walisema ukweli ndani ya
 Bunge.
Mnyika 
alisema uhuru wa Bunge wa mawazo umehojiwa nje ya Bunge kinyume cha 
kanuni, kinga na haki za Bunge jambo ambalo ni hatari kwa mustakabali wa
 Bunge.
"Mheshimiwa
 Spika, naomba kutoa hoja na wabunge wenzangu naomba waniunge mkono ili 
jambo hili liweze kujadiliwa ili Kamati ya Kinga, Haki na Madaraka ya 
Bunge imuite na ahojiwe kikamilifu," alisema Mnyika.
Baada ya 
hoja hiyo, wabunge wengi walisimama kwa pande zote bila ya kujali 
itikadi zao za vyama wakiongozwa na wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Hata 
hivyo, Spika Makinda alisimama na kuwataka waketi, ndipo akatangaza kuwa
 suala hilo haliwezi kujadiliwa bungeni, bali kamati husika itamuita 
Kisena na kumhoji.
Kisena 
hakupatikana jana kuzungumzia suala hilo na hata alipopigiwa, simu yake 
iliita bila ya kupokewa na alipotumiwa ujumbe wa maandishi hakujibu
CHANZO MWANANCHI.
CHANZO MWANANCHI.
No comments:
Post a Comment