MAREKANI KUSAIDIA NIGERIA KWA WASICHANA

Marekani 
imetangaza kwamba imetuma kikosi cha wataalamu nchini Nigeria kusaidia 
kuwatafuta wasichana takriban 200 wa shule waliotekwa nyara mwezi 
uliopita na wapiganaji wa kundi la Boko Haram.
Rais 
Barack Obama ameshutumu utekaji nyara wa wasichana hao na kusema kuwa 
mataifa yanapaswa kufanya kazi kwa pamoja ili kulikomesha Boko Haram.
"Tayari
 tumetuma kundi letu Nigeria. Wamekubali msaada wetu ambao unashirikisha
 wanajeshi, wadumishaji wa sheria na mashirika mengine ambao wanajaribu 
kutambua waliko wasichana hawa ili wawape msaada," Rais Obama alisema.
Rais 
Obama amesema kuwa jamii ya kimataifa inapaswa kutumia utekeji wa 
kikatili wa wasichana hao kama msingi wa kuungana na kuangamiza Boko 
Haram.
Nchini Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan amekubali msaada huo kama alivyosema msemaji wake, Daktari Reuben Abati.
"msaada 
huo kutoka kwa Rais Obama uliwasilishwa na Waziri wa Mashauri ya Kigeni 
John Kerry kama saa tisa alasiri hivi," Daktari Abati alisema.(P.T)
No comments:
Post a Comment