TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, May 17, 2014

Mbali na kufeli kwa msimu uliopita,hii ndiyo faida waliyopata Manchester United.

man u
Kwa mfatiliaji yoyote wa mpira wa miguu ligi ya England Manchester United ni timu ambayo haikufanya vizuri makombe yote ya msimu uliopita kitu ambacho kimekua tofauti kwa timu hiyo.
Kwenye kipindi cha miezi mitatu ya mwisho wa msimu huu Man United walipata faida ya pauni milioni 11 ikilinganishwa pauni milioni 3.6m ambazo walipata mwaka uliopita na katika msimu huo Manchester United imeripoti faida ya asilimia 20 katika kipindi cha msimu huu ambao haikufanya vizuri.
Aidha timu hiyo ilipata jumla ya pauni milioni 115.5 katika msimu uliopita ambapo asilimia kubwa ya faida hiyo ilipatikana kutoka kwa mauzo haki ya upeperushaji matangazo na mapato kutokana na tiketi za mechi.
Taarifa iliyopo ni kwamba Man United inasemekana imesaini mkataba wa miaka mitatu na kocha wa Uholanzi Louis van Gaal ambaye ndiye atakua mrithi wa David Moyes,aliyefukuzwa kazi mwezi uliyopita baada ya matokeo mabovu ya timu hizo.
Mapato yaliyotokana na hati ya upeperushaji wa mechi za timu hiyo yaliimarika kwa asilimia 64 ama pauni milioni 35.6m ilihali faida iliyotokana na uuzaji wa tiketi za mechi ilileta pauni milioni £37.1m.
Kutokana na faida hiyo kubwa Manchester united imepunguza deni lake kwa takriban pauni milioni 16 na sasa deni lililosalia ni pauni milioni £351.7m.
Kulingana na kampuni ya uhasibu ya Deloitte Football Money League, Manchester United inaorodheshwa ya nne bora miongoni mwa vilabu tajiri zaidi duniani.
Hisa za klabu hiyo ya Manchester United zilianza kuuzwa kwenye soko la hisa la New York Stock Exchange mwaka wa 2012 .

No comments:

Post a Comment