"MADENI YA WALIMU KULIPWA KABLA YA JULAI"

Bunge 
lilipitisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa 
fedha 2014/15 ya Sh bilioni 799 zikiwamo Sh bilioni 344.2 za matumizi ya
 kawaida na Sh bilioni 454.8 kwa ajili ya maendeleo.(Martha Magessa)
        
Majaliwa 
alisema madeni ya walimu yalielezwa kufikia Sh bilioni 61 na kwamba 
kumekuwa kukifanyika uhakiki, na kwa baada ya uhakiki, Februari mwaka 
huu, walilipa Sh bilioni 19.
“Lakini 
pia Machi na Aprili tayari kuna fedha nyingine zimelipwa, kwa bahati 
mbaya sikuja na takwimu hapa, lakini Serikali itahakikisha kuwa madeni 
yote yanalipwa katika mwaka huu wa fedha kabla haujamalizika,” alisema 
Majaliwa.
Aidha, 
alisema fedha nyingine za malimbikizo yakiwamo ya likizo, matibabu, 
usafiri na masomo zinalipwa kwa kupitia katika halmashauri husika.
Kuhusu 
ujenzi wa nyumba za walimu, alisema tayari nyumba 1,200 zinajengwa 
ambapo kati yake 268 zimekamilika na zimetengwa Sh bilioni 200.
Kuhusu 
fedha za chenji za rada, Naibu Waziri alisema hadi sasa zimeshanunulia 
madawati 93,988 ambayo yatagawanywa 600 kwa kila halmashauri katika 
awamu ya kwanza na awamu ya pili madawati 400.
Akizungumzia
 walimu kuwa na waajiri tofauti, alisema mwajiriwa wa walimu ni Katibu 
Mkuu Tamisemi, na katika ngazi ya mikoa wako chini ya Katibu Tawala wa 
Mkoa (RAS) na katika Halmashauri, kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya 
(DED).
Akichangia
 hoja hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na 
Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia alisema walimu wanaona unafuu 
zaidi tangu wawe chini ya Tamisemi, huku akiwataka wabunge kuacha 
kupotosha dhana ya kuchangia maendeleo.
Naye 
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, alitetea 
uamuzi wa kubadili madaraja ya ufaulu, akisema si kitu kigeni duniani. 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina 
Kombani, aliahidi kukutana na wadau ili kujadili kuundwa kwa chombo 
kimoja cha kushughulikia masuala ya walimu.
CHANZO:HABARILEO
No comments:
Post a Comment