TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, July 17, 2013

MAMA BAGHDAD AMUOMBEA MSAMAHA MWANAE KWA CHID BENZ...AOMBA WAKUTANE PAMOJA NA NAY WA MITEGO


Baada ya jana Chidi Benz kuweka wazi kuwa hategemei kumsamehe Baghdad kwa ‘blunder’ aliyoifanya ya kuwashirikisha yeye na Nay wa Mitego bila kuwaambia, mama mzazi wa Baghdad amekuja hadharani na kumuombea msamaha mwanae.

Mama huyo ameongea leo kwenye segment ya 255 kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM kuhusu nia yake ya kutaka kumaliza tofauti zilizopo kati ya mwanae na Chidi.

Mama Baghdad amekiri kuwa mwanae hakutumia akili kuchukua uamuzi huo wa kuwashirikisha wasanii wanaofahamika kuwa na uadui mkubwa kimuziki bila kufikiria madhara yake.

Amesema mwanae hakufanya jambo la busara na ndio maana ameamua kumpigia magoti Chidi ili ampe ‘second chance’ mwanae ambaye amejaribu kuomba msamaha bila mafanikio.

255 pia imezungumza na Chidi Benz aliyepo nchini Kenya kwa sasa ambaye amesema hawezi kukataa wito wa mama yake na Baghdad kwakuwa ni kama mama yake pia na amekubali kuja kukutana naye akirejea nchini.

Jana wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen ya Kenya, Chidi alisema kamwe hatokuja kumsamehe Baghdad.

Source:Mambo Mseto {Radio Citizen},Kenya

No comments:

Post a Comment