TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, July 12, 2013

CHRISTINA SHUSHO AIWEKA TANZANIA KWENYE HEADLINE AFRICA NZIMA
Shusho
Mkali wa gospel Tanzania Christina Shusho ambaye anafanya vizuri na wimbo wa Napenda, amekuwa na mwaka mzuri sana kwa upande wa kazi zake za kimuziki. Kama ulikuwa hujui mkali huyu anakubalika sana kwenye nchi za jirani ya Tanzania hasa Kenya. Miezi kadhaa iliyopita kwenye moja ya event ya utoaji wa awards kubwa za gospel nchini Kenya maarufu kama Groove Awards ambazo pia zilihidhuriwa na Rais wa kenya Uhuru Kenyatta na mke wake, Christina Shusho alishinda award ya msanii bora wa gospel wa Tanzania akiwashinda wakali wenzake kama Rose Muhando na wengine.
Kubwa zaidi ni iliyo happen wiki hii, Christina Shusho ameshinda award kubwa za gospel ambazo zinahusisha wasanii wote wa africa, Kwenye category ya Best Gospel artist from East Africa ambapo kulikuwa na wasanii lukuki ndani yake. List inahusisha wasanii kama FABRICE NZEYIMANA.ALICE KAMANDE.EXODUS-UGANDA,CHRISTINA SHUSHO TANZANIA,BLESSED SISTERS RWANDA,GEN. MANASSEH MATHIANG SOUTHERN SUDAN,JOY NKUNDIMANA BURUNDI,JULIANI,EMMY KOSGEI,MOSES “QQU” ODHIAMBO,DADDY OWEN na MARVELLOUS. Watu wangu gospel mtakuwa mashajua jinsi gani list hii ina watu wakali sana. Lakini Christina Shusho anastahili pongezi za pekee kwa kushinda tuzo hii na kuiwakilisha Tanzania vema kwenye anga ya muziki wa injili.

No comments:

Post a Comment