TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, July 12, 2013

WANAUME WA KENYA WAZIDI KUNYANYASWA.....MWAMAUME MWINGINE APIGWA VIBAYA NA MKEWE


Ni ngumu kumuona mwanaume akitokwa machozi kama hivi…. hii imetokana na mke wake kumpiga makofi hadharani kwenye mji wa Meru nchini Kenya ambapo Mwanamke huyo alikua anadai jamaa kamkana, japo anasisitiza kwamba ni mume wake na ndio baba wa watoto mapacha akiwemo mmoja alienae mgongoni, Mwanaume alikataa kabisa na kusema hata watoto sio wake.
Taarifa ambayo imerushwa na KTN Kenya, ni kwamba alichotaka Mwanamke ni Mwanaume huyo akubali tu kwamba ni mume wake na pia ndio baba watoto wa mapacha hao… lakini Mwanaume aliapa kabisa kwamba hausiki kwenye upande wowote, hicho ndio kilichompa hasira Mwanamke na kuanza kumpiga na baadae pia kusaidiwa kupiga na Mwanamke aliekua nae.

Kenya imekua kwenye mfululizo wa kesi za Wanawake kupiga waume zao nyumbani na hadharani pale wanapokosana ambapo February 2012 Umoja wa Wanaume Kenya ulitangaza kususia kula majumbani kwa wiki moja na kununua chakula hotelini mpaka Serikali itakapoingilia usawa wa Wanaume na kuhakikisha tabia ya Wanawake kupiga Waume zao inamalizwa.

No comments:

Post a Comment